HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 07, 2019

TIGO, MO, MILVIK WANG'ARA TUZO ZA BIMA

NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

MILVIK  Tanzania kwa kushirikiana na Tigo Pesa, Resolution na Mo wameshinda tuzo ya huduma ya Bima yenye ubunifu zaidi kupitia huduma yake ya Bima Mkononi.
 
Meneja Mkuu wa Milvik, Berengere Lavisse, alisema wanajivunia kutoa huduma rahisi na nafuu kwa wateja wa kipato cha chini kwa ushirikiano na Tigo Pesa, Resolution na Mo. 

"Kupitia bima yetu mpya ya kulazwa na watoto, wazazi wanaweza kuwalinda watoto wao kwa matibabu ya kulazwa kwa shilingi 750 tu kwa mwezi kwa kila mtoto, kwa kutumia simu zao, bila kujaza fomu za makaratasi na kwa mfumo rahisi wa malipo kupitia Tigo Pesa.,"

"Tunawashukuru wateja wetu ambao wameendelea kutuamini katika kulinda hatima za familia zao na tunatarajia kuwaletea huduma zenye ubunifu zaidi katika mwaka 2020.”alisema Lavisse
 
Alisema kuhusu  bima mkononi kuna huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja  na Bima mkononi ya kulazwa kwa sh 1500 kwa mwezi, Bima mkononi ya ajali binafsi shilingi  1,000 na bima mkononi ya maisha shilingi  1,500, au kifurushi chenye bima zote kiitwacho bima mkononi Faraja Yangu. 

Mnamo mei mwaka huu, Milvik ilizindua mfumo mpya wa malipo unaowezesha wateja kukatwa malipo kila mwezi kutoka kwenye akaunti zao za Tigo Pesa, na kuifanya Bima Mkononi kuwa huduma ya gharama nafuu na rahisi kutumia kwa watumiaji wa kipato cha chini.

Imeelezwa kuwa wateja wanaweza kudai fidia ya shilingi  40,000 kwa kila usiku watakaolazwa hospitali, shilingi 3,000,000 iwapo mteja atapatwa na umauti au ulemavu wa kudumu kutokana na ajali, na shilingi 1,000,000 kwa umauti wa sababu yoyote.

Kutokana na ushirikiano wake na Tigo, Milvik ina kituo cha huduma kwa wateja jijini Dar es Salaam kinachowawezesha kuwafikia watumiaji kote nchini hivyo kukuza wigo wa huduma na kuendelea kutoa huduma za gharama nafuu.
 
Na jinsi ya kujiunga  kupitia simu yako ya mkononi kwa kupiga *148*15# au kupitia huduma kwa wateja kwa kupiga simu ya bure 0659071001. 

No comments:

Post a Comment

Pages