HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 16, 2020

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA "CHANJA, LIPA, SEPA" NA TEMBOCARDVISA

Benki ya CRDB leo Januari 16, 2020 imezindua rasmi huduma ya “Chanja, Lipa, Sepa” kwa maduka yote yanayokubali malipo ya kadi ambapo wateja watakaofanya malipo kwa TemboCardVisa na  SimBankingVisa wataweza kufurahia punguzo la bei hadi asilimia 60 kwa manunuzi ya kuanzia shilingi 30,000 katika maduka na migahawa mbalimbali hapa nchini.
 
Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif, akizungumza na  waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma ya “Chanja, Lipa, Sepa” ya Benki ya CRDB kwa kutumia TemboCardVisa. Kampeni hiyo ilifanyika leo kwenye Duka la Miniso, Mlimani City, jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara na Kadi wa Benki ya CRDB, Farid Seif , akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kufanya malipo kwa kutumia kadi ijulikanayo kama “Chanja, Lipa, Sepa” uliofanyika leo kwenye maduka ya GSM na Miniso, yaliyopo Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages