HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 14, 2020

MAALIM SEIF, KIGOGO ACT - WAZALENDO WAKAMATWA NA POLISI ZANZIBAR


 Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, akiwapungia mkono wananchi waliojitokeza wakati alipoitwa Kituo cha Polisi Wete, Pemba.
  Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, akiwapungia mkono wananchi waliojitokeza wakati alipoitwa Kituo cha Polisi Wete, Pemba.
 Baadhi ya wafuasi wa Maalim Seif Sharif Hamad wakimsubiri wakati akihojiwa na Polisi.


Na Talib Ussi, Zanzibar
Jeshi la Polis Mkoa wa Kaskazini Pemba limewaachia kwa dhamana Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Habari, Mawasiliano ya Umma, Salim Biman, kwa madai ya kufanya mkusanyiko kinyume na sheria katika eneo la Kiuyu Mbuyuni Wilaya ya Micheweni.
Akizungumza na waandishi wa habari mara ya kumaliza kumhoji Maalim Seif, Kamanda wa Polisi Kaskazini Pemba, Juma Sadi Khamis, alisema waliwaita viongozi hao kwa kufanya mkutano wa hadhara Desemba 9, 2019 huku wakijua mikutano yote imezuiwa.
“Mkutno huo ulikuwa wa ndani, lakini waliufanya wa wazi jambo ambalo halikuwa na uhalali wa kisheria”, alieleza Khamis.
Alisema kuwa viongozi hao wote wameaachiwa kwa dhamana bila ya kutaja siku ya kurudi kituoni na kueleza kuwa na jalada wameshalipeleka kwa DPP kwa hatua zaidi.
Kwa upande wake Maalim Seif alisema anashangaa kuaambiwa kuwa wamefanya mkutano wa hadhara kwa kile alichoeleza kuwa mkutano wao ulikuwa wa ndani na nje kufunga maturubali ili kuwadhibiti watu wao.
“Sisi tumepangua hoja zote kwa sababu hazina mashiko, watu wetu sisi wote walikuwa ndani na ambao walikuwa nje hatukuwa na dhamana nao”, alisema maalim Seif.
“Tumewaambia kuwa Polisi ule sio mkutano wa nje, kwa sababu mkutano wa nje lazima utangazie watu kila kona lakini sisi hatujatangazia mtu” aliendelea.
Alieleza kuwa alipokwenda Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Dk. Bashiru Ali, kisiwani baadhi ya barabara zilifungwa lakini jeshi hilo halikueleza chochote na badala yake wanafanyakazi ya CCM kudhibiti mtu ambaye hawamuwezi.
“Kwa hiyo nakuombeni wananchi msiwe na wasiwasi sisi tuko salama na tutaendelea kufanya shuhuli zetu kisiasa kwani zipo kisheria”,  alisema Maalim Seif.
Baada ya kutoka kituoni hapo Maalim Seif alipokelewa na wanachama na wananchi waliokuwa nje ya kituo.
Mamia ya wafuasi wa chama hicho walijitokeza nje ya kituo wakipiga mayowe ya kumtaka kiongozi wao, na Jeshi la Polisi kuwaamuru waondoke bila kufanikiwa.
"Tunalishauri Jeshi la Polisi liache kutumika kisiasa mwenendo wake ni dhahiri linatumiwa na CCM.
“Sisi kazi yetu ni kulinda kituo chetu hatuwezi kuwaingilia watu walio nje ya kituo, ambao wana shauku na viongozi wao”, aliendelea.
Kwa upande mwingine Katibu wa Mipango na Wanachama wa chama hicho, Omar Ali Shehe na Katibu wa Mkoa wa Kusini Pemba na waliitwa na Jeshi hilo mkoni humo kujibu hoja kama hizo.

No comments:

Post a Comment

Pages