HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 09, 2020

TMA yatangaza mwezi kupatwa kwa saa 4

Na Irene Mark

MAMLAKA ya hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza tukio la kupatwa kwa mwezi kwa zaidi ya saa nne kuanzia saa 2:07 usiku wa Januari 10 hadi saa 6:17 usiku wa kuamkia Januari 11,2020.

Taarifa ya kupatwa kwa mwezi ilitolewa Dar es Salaam leo Januari 9, 2020 na Meneja wa Utabiri wa Kituo Kikuu cha Utabiri, Samuel Mbuya na kusema ni tukio nadra kutokea kwa muda mrefu hivyo kuwataka watanzania kushudia sayansi hiyo ya anga.

"Tukio hili litaonekana kwa sehemu kubwa kwenye nchi ambazo muda huo utakuwa usiku hasa Ulaya, Asia, Australia na Afrika...hili tukio huonekana wakati dunia, mwezi na jua vikikutana kwenye mstari mmoja mnyoofu.

"Mwezi huanza kupungua mng'ao wake na kuwa giza kabisa kwenye uso wa dunia kwa muda kisha hurudi kwenye hali yake ya kawaida, hakuna athari kubwa zinazoweza kutokea ingawa kuna uwezekano wa kuongezeka kwa kina cha maji baharini kwa sababu ya mvutano kati ya maji na mwezi kwenye bahari," alisema Mbuya.

Alitumia muda huo kuwashauri wanafunzi wa masomo ya sayansi kufuatilia tukio hilo la kidunia na kujifunza zaidi kuhusu sayansi ya anga.

No comments:

Post a Comment

Pages