HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 23, 2020

COASTAL UNION YAIVIMBIA YANGA

Mchezo huo wa kuvutia kwa pande zote mbili, ulifanyika leo Februari 23, 2020 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga, na kuwafanya mabingwa hao mara 27, kutoka uwanjani wakiwa hawaamini.
Sare hiyo ni ya nne mfululizo kwa Yanga, ambayo imekuwa na matokeo ya ovyo hivi sasa na kujiweka sehemu mbaya ya kuweza kutwaa taji hilo msimu huu.
Wanajangwani hao walianza kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City, kisha Tanzania Prisons (0-0), Polisi Tanzania (1-1) na hii ya Coatal Union.
Mwenendo huo mbovu wa Yanga, unawafanya watani zao, Simba kutanua kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo, kwa kuwaacha kwa ‘gepu’ kubwa la pointi.
Hivyo basi, matokeo hayo yanawafanya kuendelea kushika nafasi ya nne, ikiwa na pointi 41, wakicheza michezo 22, lakini wakiwa na faida ya viporo viwili.
Lakini imeachwa pointi 21 na vinara wa ligi hiyo, Simba ambayo inaongoza msimamo huo wakiwa na pointi  62, baada ya juzi kushinda mechi yake dhidi ya Biashara United ya Mara.
Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa pande zote mbili, kwa kutengeneza nafasi nyingi za mabao ambazo safu zao za ushambuliaji zilishindwa kuzitumia.
Katika kipindi cha kwanza, Yanga ndio iliutawala mchezo, hadi kumiliki mpira kwa asilimia 55 kwa 45 za Coastal Union inayonolewa na Kocha Juma Mgunda.
Kipindi cha pili Coastal Union ilizinduka zaidi hadi kumaliza dakika 90, wakiwa sawa uwiano wa umiliki wa mpira wakiwa na 50 kwa 50.
Ni mchezo ambao ulikuwa bora, lakini jambo ambalo lilikosekana na upachikaji wa mabao tu, kwa vile safu zote za ushambuliaji zilikosa kuwa makini.
Matokeo mengine ya leo, Tanzania Prisons waliifumua Lipuli FC, mabao 2-0, kwenye Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya, wakati Alliance FC wakilazimishwa sare ya 1-1 na Singida United, Uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza.
Golikipa wa Yanga, Metacha Mnata, akimzuia winga wa Coastal Union ya Tanga, Issa Said, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Timu hizo zilitoka suluhu. (Picha na Coastal Union).



Na Mwandishi Wetu, Tanga
MABINGWA wa kihistoria, Yanga SC, imezidi kupunguzwa kasi ya kutwaa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL), msimu huu, baada ya jana kulazimisha suluhu dhidi ya wenyeji, Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’ ya Tanga.
Mchezo huo wa kuvutia kwa pande zote mbili, ulipigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga, na kuwafanya mabingwa hao mara 27, kutoka uwanjani wakiwa hawaamini.
Sare hiyo ni ya nne mfululizo kwa Yanga, ambayo imekuwa na matokeo ya ovyo hivi sasa na kujiweka sehemu mbaya ya kuweza kutwaa taji hilo msimu huu.
Wanajangwani hao walianza kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Mbeya City, kisha Tanzania Prisons (0-0), Polisi Tanzania (1-1) na hii ya Coatal Union.
Mwenendo huo mbovu wa Yanga, unawafanya watani zao, Simba kutanua kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo, kwa kuwaacha kwa ‘gepu’ kubwa la pointi.
Hivyo basi, matokeo hayo yanawafanya kuendelea kushika nafasi ya nne, ikiwa na pointi 41, wakicheza michezo 22, lakini wakiwa na faida ya viporo viwili.
Lakini imeachwa pointi 21 na vinara wa ligi hiyo, Simba ambayo inaongoza msimamo huo wakiwa na pointi  62, baada ya juzi kushinda mechi yake dhidi ya Biashara United ya Mara.
Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa pande zote mbili, kwa kutengeneza nafasi nyingi za mabao ambazo safu zao za ushambuliaji zilishindwa kuzitumia.
Katika kipindi cha kwanza, Yanga ndio iliutawala mchezo, hadi kumiliki mpira kwa asilimia 55 kwa 45 za Coastal Union inayonolewa na Kocha Juma Mgunda.
Kipindi cha pili Coastal Union ilizinduka zaidi hadi kumaliza dakika 90, wakiwa sawa uwiano wa umiliki wa mpira wakiwa na 50 kwa 50.
Ni mchezo ambao ulikuwa bora, lakini jambo ambalo lilikosekana na upachikaji wa mabao tu, kwa vile safu zote za ushambuliaji zilikosa kuwa makini.
Matokeo mengine ya jana, Tanzania Prisons waliifumua Lipuli FC, mabao 2-0, kwenye Uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya, wakati Alliance FC wakilazimishwa sare ya 1-1 na Singida United, Uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment

Pages