HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 13, 2020

Makuwa akerwa na wanaodai Katiba, NEC huru

Mkurugenzi wa The Society Awareness, Felix Makuwa.



NA MWANDISHI WETU
 
MKURUGENZI wa Taasisi ya  The Society Awareness, Felix Makuwa, amesema kauli za viongozi wa vyama vya siasa na wastaafu kudai Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi wakati huu hazina afya kwa maendeleo ya nchi kwa sasa.

Makuwa ametoa kauli hiyo kwenye taarifa aliyoitoa jana jijini Dar es Salaam kwa vyombo vya habari yenye kichwa cha habari kinachosema ‘Uhusiano tata ya Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba na upinzani (Ukawa)

Mkurugenzi huyo alianza kwa kuwatahadharisha Watanzania wawe macho kuhusu kauli tata zinazozuka sasa wakati huu ambao nchi inajiandaa na uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani.

Makuwa ambaye alijitambulisha kuwa ni mwanaharakati alisema kwa siku za karibuni baadhi ya watu wamekuwa wakitumia majukwaa kudai katiba na tume huru jambo ambalo linaibua maswali mengi.

Alisema katika kilele cha miaka 58 ya uhuru jijini Mwanza, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe alizungumzia suala la maridhianbo ya kisiasa na baadae akamuandikia barua Raisi kulalamikia mambo mbalimbali.

“Baadhi ya mambo hayo ni tume huru ya uchaguzi huku wakijua kuwa tume zote mbili (NEC) na (ZEC) ni huru na ndio maana ndani ya Bunge kuna wabunge wa upinzani.

Nimeshangazwa mda sio mfupi baada ya barua hiyo ya Chadema  kwenda kwa Rais, ameibuka aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Jaji mstaafu Warioba na kuzungumzia hitaji la katiba mpya.

Makuwa alisema Warioba alisimamia mchakato wa Katiba ambayo ilikwama hivyo hana sababu ya kuanzisha habari za Katiba mpya kwa kuwa Katiba iliyopo inakidhi vigezo kwa kusimamia haki na amani tangu kupatikana kwa uhuru.

Mwanaharakati huyo alihoji maswali iwapo tume hakuna wabunge wamepatikanaje ni kwanini sasa ndio wanaibuka wanaodai tume huru na kwanini sasa yanaonekana mahusiano ya watu wa Chadema na CCM kudai kitu kimoja.

Alitolea mfano kuwa Warioba  alipewa nafasi katika tume hio na akazalisha rasimu ambayo ililenga kuvunja amani  ya nchi kama serikali haingekuwa makini, ingawa rasimu hiyo ilikuwa rafiki wa wapinzni.

“Hivi jamani kama kuna jambo zuri linalohusu Katiba, kiongozi mkuu kama Warioba aliona shida gani kwenda kumuona Rais John Magufuli na kumshauri bila kukimbilia vyombo vya habari na pia huu ujasiri kuiyelekeza nchi kupitia vyombo vya habari unatoka wapi?.

Mwanaharakati huyo amewaomba na kuwaasa Watanzania wawe macho na wajihadhari na watu hawa  ambao wapo tayari kupindisha ukweli na amani ya nchi  kwa kisingizio cha Katiba mpya au tume huru ya uchaguzi.

Makuwa alisema tume huru au katiba mpya sio muarubaini wakupata viongozi bora au wachapa kazi bora.

Aidha alimshauri Msajili wa Vyama vya Siasa kuchukua hatua dhidi ya vyama na wanasiasa ambao amedai wanapotosha umma kwa maslahi yao.

No comments:

Post a Comment

Pages