Mtafiti wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), akiweka sampuli kwenye mashine ya kuchambua vinasaba ya Oxford MinION nanopore. (Na Mpiga Picha Wetu).
Na Suleiman Msuya
TUME ya Taifa
ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Mfuko wa utafiti wa
Afrika Kusini (National Research Foundation) na Taasisi Oliver Tambo Africa
Research Chairs Initiative, inatarajia kuwezekeza Dola za Marekani milioni 2
ambazo ni zaidi na shilingi bilioni 4 katika Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) na
Nelson Mandelea Arusha ili kufanya utafiti wa virusi na dawa za malaria.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, COSTECH, Profesa Mohamed
Sheikh wakati akizungumza na Habari Mseto Blog.
Prof.
Sheikh alisema Tanzania inatarajia kupata fedha za utafiti ya kiasi cha dola
milioni 2 za Marekani hivyo wamelazimika kuelekeza kwenye utafiti huo ili
kuweza kutatua changamoto mbali mbali ndani ya nchi zikiwemo tafiti za magonjwa
yanasobabishwa na virusi na malaria.
Alisema
magonjwa ambayo yanatokana na virusi yanasumbua duniani kote hivyo ni vema
kuwekeza katika utafiti ili kuweza kusaidia jamii.
Sheikh
alisema ushahidi ni hali ilivyo sasa ambapo dunia inateswa na kirusi cha corona
kinachosababisha ugonjwa wa COVID-19.
“Fedha
hizo za utafiti Dola za Marekani milioni 2 zinatolewa na COSTECH, zinatarajiwa
kuwekezwa katika vyuo vya SUA na Nelson Mandela ambapo watafiti wetu kwa kushirikiana
na Tume wataweza kuja na majibu kuhusu maradhi haya yanayosumbua jamii”
alisema.
Kaimu
Mkurugenzi huyo alisema SUA watatafiti kuhusu magonjwa yanahusu virusi
vinavyosababishwa na wanyama ambavyo vinaweza pia kuathiri afya ya binadamu.
Alisema kwa
upande wa Nelson Mandela watajikita katika utafiti wa kupata tiba ya malaria kwa
kutumia utaalamu wa ‘nano-technology’ambayo itaweza kupunguza au kuondoa changamoto hiyo.
Alisema
tume inashirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje kuratibu utafiti unaowezesha
watafiti wazawa ambao wanatatua matatizo ya ndani.
Kaimu
Mkurugenzi huyo alisema matarajio yao ni kutumia majibu ya utafiti huo kwa nchi
zote hasa za Afrika ambazo zitahitaji ili kuweza kuokoa jamii na magonjwa
yanayosabishwa na vurusi na ugonjwa wa malaria.
Prof.
Sheikh alisema katika juhudi za kuratibu utafiti wanaendelea kushirikiana na
taasisi mbalimbali ikiwemo Kituo cha Kimataifa Uhandisi Jeni na Bioteknolojia (ICGEB),
kilicho na makao makuu yake nchini Italia ili kuhakikisha wanabadilisha jamii
ya Kitanzania kimaendeleo na uchumi.
Sheikh
alisema pia wamekuwa wakipata ufadhili wa masomo katika ngazi ya uzamili na
uzamivu katika maeneo mbalimbali katika kada tofauti kama magonjwa ya afya,
akili na mengine.
Aidha,
alisema wanatumia watafiti waandamizi ambapo wanashindanishwa na nchi
mbalimbali ambazo wanashirikiana nazo.
“Ushirikiano
wetu na ICGEB umekuwa na manufaa mengi kwa Tanzania ikiwa ni pamoja na watafiti
wa kitanzania kupata zaidi ya dola 350,000 za Marekani na huku COSTECH imechangia
ada ya uanachama wa dola 5,000 kwa mwaka alisema.
Lengo la Tume ni kutumia uvumbuzi katika nyanja za sayansi na teknolojia
ili kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa na maisha mazuri na afya njema.
No comments:
Post a Comment