HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 02, 2020

Madiwani Waazimia kuwawajibisha watumishi wanaokula njama na wakwepa ushuru

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mheshimiwa Steven Kayogolo akitoa maagizo ya mwisho kwa Afisa utumishi na  Mwanasheria wa Halmashauri hiyo (hawapo pichani) juu ya kutafuta vifungu vya kanuni za kuwawajibisha watumishi wakati akifunga baraza la madiwani. 


Na Mwandishi Wetu

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi limeazimia kuzitumia kanuni za utumishi wa umma zinaoelezea adhabu inyaotolewa kwa watumishi ambao hawawajibiki ipasavyo kwa mwajiri wao katika kuhakikisha wanakusanya ushuru kwenye maeneo yao waliyopangiwa na hatimae kuongeza mapato ya halmashauri hiyo iliyopo Mkoani Rukwa
Kauli hiyo imetolewa na kaimu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mh. Steven Kayogolo wakati akifunga baraza hilo la robo ya pili ya mwaka wa fedha 2019/2020 na kuongeza kuwa baraza hilo limekuwa likitumia njia kadhaa ambazo hadi sasa hazijawaletea matunda huku mapato ya halmashauri hiyo yakiendelea kudemadema jambo ambalo linaathiri utendaji kazi wa halmashauri hiyo.
“Kwahiyo tutatafu kama watatu hivi “demo” tunajaribu mitambo, kwahiyo watu wakae wajitathmini, wapo watu wanaosimamia mageti, tunataarifa tunazo ambazo watu wanafanya udanganyifu kwenye mapato, sasa mimi nawaambia kuna mtu ataruhusu gari iondoke, tutaikamata, tukimkamata huyo haponi, huo ndio msimamo wa halmashauri,” Alisisitiza.
Wakati akitoa salamu za katibu Tawala wa mkoa katika baraza hilo Afisa wa Serikali za Mitaa wa Mkoa wa Rukwa Abinus Mgonya alisikitishwa kwa kuporomoka kwa ukusanyaji wa mapato ya halamshauri hiyo hali ambayo ilikuwa tofauti ukilinganisha na mwaka wa fedha wa 2018/2019 katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai hadi januari.
Alisema kuwa hali ya ulinganifu wa kipindi hicho siyo nzuri kwa halmashauri ya Nkasi na kuongeza kuwa halmashauri hiyo imekuwa ya mwisho kati ya halmashauri nne za mkoa huo ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ikiongoza katika ukusanyaji wa mapato ikifuatiwa na halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, huku Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo ikishika nafasi ya tatu.
“Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kwa mwaka 2019 mwezi Februari makusanyo yalikuwa ni shilingi 1,517,348,839 sawa na 66% ya makadirio ya Shilingi 2,000,304,000 kwa mwaka 2020 hadi mwezi Januari, halmashauri ya wilaya ya Nkasi ilikuwa imekusanya shilingi 919,830,000 na hii ni kwa mujibu wa takwimu tulizonazo pale mkoani kabla ya halmashauri haijafanya usuluhishi wa mifumo ya matumizi na mifumo ya mapato ndio maana sisi pale mkoani inasomeka 36.9%,” Alisema
Na kusisitiza kuwa Halmashauri hiyo imeteremka kimapato kutoka 66% mwaka jana kipindi kama hicho hadi kufikia 36.9% ambapo ni sawa na anguko la asilimia 30% na kutanabaisha kuwa kutokana na anguko hilo ni dhahiri kuwa jambo linaitafuna halmashauri hiyo na hivyo kuwataka waheshimiwa madiwani kujifanyia tathmini
Halikadhalika alitilia makazo suala la kuziwasilisha benki fedha zote zilizokusanywa kabla ya kupangiwa matumizi na halmashauri ili ziweze kusomeka katika Mfumo wa Taarifa za Ukusanyaji Mapato wa Serikali za Mitaa (LGRCIS) na kuongeza kuwa hadi Januari 31, fedha ambazo zilikuwa mikononi mwa wakusanya mapato na hazijawasilishwa benki kwa halmashauri ya Wilaya ya nkasi ni shilingi 101,947,971 na baada ya kufanyika usuluhishi kwa mwezi Februari shilingi 73,954,991 zimeingizwa benki na hivyo kuwataka kuelekeza nguvu katika vyanzo vinavyochangia Zaidi mapato.
Manispaa ya Sumbawanga kwa mwaka 2019 mwezi Februari makusanyo yalikuwa shilingi bilioni 2.1 sawa na 98.1% ya makadirio ya shilingi bilioni 2.2 na Januari, 2020 imekusanya shilingi bilioni 1.7 sawa na 73% ya makadirio ya shilingi bilioni 2.4, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kwa mwezi Februari 2019 makusanyo yalikuwa shilingi milioni 801 sawa na 35% ya makadirio ya shilingi bilioni 2.3 na Januari 2020 imekusanya shilingi bilioni 1.3 sawa na 54% ya makadirio ya shilingi bilioni 2.3 na Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa mwezi Februari 2019 makusanyo yalikuwa ni shilingi milioni 720.9 sawa na 36.05% ya makadirio ya shilingi bilioni 2. Na Januari 2020 imekusanya shilingi milioni 865.2 sawa na 46% ya makadiririo ya shilingi bilioni 1.8.

No comments:

Post a Comment

Pages