HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 08, 2020

UYUI YATOA MKOPO WA MILIONI 43 KWA VIKUNDI 13

NA TIGANYA VINCENT
 
HALMASHAURI ya Wilaya ya Tabora (Uyui) imetoa mikopo ya shilingi milioni 43 kwa vikundi13 kwa ajili ya kuviwezesha katika uzalishaji mali.

Mikopo hiyo imekabidhiwa kwa vikundi jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri kwa niaba ya Halmashauri  hiyo wakati wa kikao cha Baraza Madiwani.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Hemed Magaro alisema kuwa wametoa kiasi cha shilingi milioni 19 kwa vikundi sita vya wanawake, vikundi 6 vya vijana vimekopeshwa milioni  19 na kikundi kimoja cha walemavu kimekopeshwa shilingi milioni 5.

Alisema mkopo huu unafikisha shilingi milioni 135.5 ambazo zimeshatolewa katika vikundi kama sehemu asilimia 10 ya mapato yake ya ndani.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mwanri alivitaka vikundi vilivyokopeshwa kuhakikisha wanatumia fedha za mikopo walizopata katika shughuli za uzalishaji mali kwa ajili ya kuboresha maisha yao.

Alisema fedha walizokopehwa ni lazima wazirejeshe katika muda waliokubaliana na uongozi wa Halmashauri ili ziweze kusaidia vikundi vingine.

No comments:

Post a Comment

Pages