HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 09, 2020

Wanawake CUF wamchangia fedha Prof.Lipumba

Makamu Mwenyekiti  Jumuiya ya wanawake wa Chama cha Wananchi CUF ambaye pia ni mbunge viti maalumu aliyemaliza muda wake  Mkoa wa Kigoma Kiza Mayeye kushoto akizungumza na wanahabari


Na Asha Mwakyonde

 
WANAWAKE wa Jumuiya ya Chama cha Wananchi (CUF), wamechangia kiasi cha Sh. Milioni 1, Mwenyekiti wa chama hicho Prof. Ibrahimu Lipumba  kwa ajili ya kuchukulia fomu ya kugombea nafasi ya urais Oktoba mwaka huu.
 

Haya yamesemwa jijini Dar es Salaam jana na Makamu Mwenyekiti  Jumuiya ya wanawake wa Chama hicho  ambaye pia ni mbunge viti maalumu aliyemaliza muda wake  Mkoa wa Kigoma Kiza Mayeye  amesema wanaamini Prof. Lipumba anafaa.


Kiza amesema baada ya Mwenyekiti huyo Prof. Lipumba kuamua kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya urais Oktoba mwaka huu wao kama wanawake waliona ni vema wakachanga kwani wanaamini ndiye rais anayefaa kushika dola.


Amesema kuwa wao kama wanawake wa jumuiya ya chama hicho wanaamini Prof. Lipumba ndiye tumaini lao ndiyo maana wamemua kuchanga fedha kwa ajili ya  kuchukulia fomu.
 

Amesema kuwa wanawake wa chama hicho kwa kushirikiana wamechanga  na kupata kiasi cha Sh. Milioni  1 na kumkabidhi Prof. Lipumba  ili aende jijini Dodoma kuchukua fomu hiyo. 'Sisi kama wanawake wa chama cha wananchi Cuf tutakuwa  pamoja naye kumpeleka jijini Dodoma kuchukua fomu ya urais Agasti 10 mwaka huu,' amesema Kiza.


Ameongeza kuwa kampeni zitakapoanza watakuwa na gombea wao wa kiti cha urais  na kwamba watahakikisha wanatafuta kura  mchana na usiku ili kuhakikisha chama hicho kinashika dola.

No comments:

Post a Comment

Pages