HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 25, 2020

UWT MKOA WA DODOMA, NEEMA MAJULE AELEZEA JINSI WALIVYOJIPANGA KUWEKEZA MIRADI HADI KWENYE KATA

Mwenyekiti wa  Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT-CCM) Mkoa wa Dodoma, Neema Majule  ameelezea mambo mbalimbali ikiwemo jinsi uongozi wake ulivyowezesha ujenzi wa  miradi miwili ya Shule ya Awali na jengo la maduka Kilimani, jijini Dodoma,  na mipango mingine ya ujenzi katika viwanja sita walivyovikomboa baada ya kudhurumiwa.

Pia mama huyo jabali, amewapongeza wanawake kwa kufanikisha ushindi mkubwa wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Vilevile ameupongeza uongozi wa juu wa chama hicho kinachoongozwa na Rais John Magufuli kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa miaka mitano ya kuiletea Tanzania mafanikio jambo ambalo pia limechangia CCM kupata ushindi mkubwa.

No comments:

Post a Comment

Pages