HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 09, 2021

VIONGOZI TENDENI HAKI: MAALIM SEIF

 Makamu  wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amewata viongozi kutenda haki kwa Wazanzibar wote bila ya kujali tofouti zao.

 

Alisema  kama wananchi na viongozi wao watashirikiana itakuwa chachu ya kusukuma mbele gorudumu la Maedeleo miongoni mwa Wazanzibar.

 

Maalim Seif alisema hayo katika msikiti wa Jumuiya ya waarabu uliopo Rahaleo Unguja akiungana na waimini wa Dini ya Kiislam kuswali swala ya Ijumaa.

 

Aliwataka viongozi wote waliochaguliwa na wale wateule kupiga vita ubaguzi wa aina yoyote katika kuwahudumia wananchi.

 

“Tukifanyakazi kwa pamoja nakuhakikishieni maendeleo ni rahisi sana” alisema Malim Seif.

 

Sambamba na hilo amewataka waumini Dini ya Kiislam kuiombea Dua Zanzibar ili umoja uliopo udumu.

 

Akizugmzia kuhusu ajira uwepo wa utulivu ni muhimu kwa ushiriiana an sekta binafsi kuondoa changamoto ajira Viwani Zanzibar.

Kama tikuvutana tutachelewa kupata maedeeo lakini sisi Wazanzibar tumelijua hilo ndio maana tukawa na SUK.

 

Alieleza kuwa changamoto ya ajira ni kubwa ambayo huipata wahitimu wa vyuo vya elimu ya Juu mbali mbali Tanzania.

Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipaga kutatuwa Changamoto inayowakabili akina mama na Vijana ya ajira na kuwataka wananchi wote kushiriki kwa hali na mali katika shuhuli za Maendeleo hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages