Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi 
na Usalama wa mkoa huo, Amos Makalla, akizungumza kuhusiana na watu wanaojihusisha na 
ujambazi na kuliagiza Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam 
kuwashughulikia kikamilifu majambazi na vibaka jijini humo.  
 Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Mkuu
 wa Mkoa wa Dar es Salaam  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi 
na Usalama wa mkoa huo , Amos Makalla amewaonya watu wanaojihusisha na 
ujambazi na kuliagiza Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam 
kuwashughulikia kikamilifu majambazi na vibaka jijini humo. 
Hatua
 hiyo imekuja siku chache baada ya kutokea matukio ya ujambazi katika 
eneo la Mbezi ambapo majambazi walisababisha kifo cha mtu mmoja 
aliyekuwa akitoka benki kuchukua fedha na kwamba tukio la pili lilitokea
 Mabibo na kwamba majambazi walimjeruhi mfanyabiashara katika harakati 
za kutaka kumpora fedha zake.
Aidha,
 amewataka watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha 
polisi mara moja na kwamba watakaokaidi watachukuliwa hatua kali za 
kisheria.
RC huyo ameliagiza jeshi hilo kuanza kwa operesheni ya kufagia watu wote wanaofanya uhalifu mkoani humo ambapo amewaomba wazazi kufuatilia mienendo ya watoto kwa kuwakanya endapo wanashiriki waache kushiriki.
Amesema kwakuwa uzoefu unaonyesha wahalifu hutumia silaha kujeruhi na kusababisha vifo, hivyo ni vyema jeshi hilo likawachukulia hatua kikamilifu kabla hawajazitumia katika uporaji na mauaji wakati wakiwa kwenye matukio ya ujambazi.
Amewahikikishia wananchi usalama na kuwataka kuendelea kufanya shughuli zao kama kawaida kwani vyombo vya ulinzi na usalama viko macho kuwashughulikia wale wote wenye nia ya kuhatarisha usalama wa wakazi na mali zao.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Camilius Wambura amesema Katika msako ulioanza Mei 21 hadi Mei 25 wamefanikiwa kuwakamata Majambazi na vitu mbalimbali ikiwemo magari manne, pikipiki moja, bunduki moja, laptop na vifaa vinginevyo.
Aidha Kamanda Wambura amesema kuwa maagizo yaliyotolewa wameyapokea kwa mikono miwili na watayafanyia kazi kwa ufanisi mkubwa.
RC huyo ameliagiza jeshi hilo kuanza kwa operesheni ya kufagia watu wote wanaofanya uhalifu mkoani humo ambapo amewaomba wazazi kufuatilia mienendo ya watoto kwa kuwakanya endapo wanashiriki waache kushiriki.
Amesema kwakuwa uzoefu unaonyesha wahalifu hutumia silaha kujeruhi na kusababisha vifo, hivyo ni vyema jeshi hilo likawachukulia hatua kikamilifu kabla hawajazitumia katika uporaji na mauaji wakati wakiwa kwenye matukio ya ujambazi.
Amewahikikishia wananchi usalama na kuwataka kuendelea kufanya shughuli zao kama kawaida kwani vyombo vya ulinzi na usalama viko macho kuwashughulikia wale wote wenye nia ya kuhatarisha usalama wa wakazi na mali zao.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Camilius Wambura amesema Katika msako ulioanza Mei 21 hadi Mei 25 wamefanikiwa kuwakamata Majambazi na vitu mbalimbali ikiwemo magari manne, pikipiki moja, bunduki moja, laptop na vifaa vinginevyo.
Aidha Kamanda Wambura amesema kuwa maagizo yaliyotolewa wameyapokea kwa mikono miwili na watayafanyia kazi kwa ufanisi mkubwa.
Kamanda
 huyo amewaonya wahalifu wanaoshindana na vyombo vya ulinzi na usalama 
kuacha kujidanganya kwani mkono wa sheria ni mrefu.
 
 


 
 

 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment