Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba, akimpatia vitabu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dk. Faustine Ndugulile alipotembelea banda la mfuko huo kwenye maonesho ya 45 ya DITF.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dk. Faustine Ndugulile, akizungumza na waandishi wa alipotembelea banda la Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)huo kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa.
Na Selemani Msuya
MFUKO
wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), unatarajia kutumia shilingi bilioni
32 katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 kwa ajili ya kupeleka huduma ya
mawasiliano pembezoni mwa Tanzania na mashuleni.
Hayo yamesemwa
na Mtendaji UCSAF Justina Mashiba wakati akizungumza na gazeti hili
kwenye kwenye Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam
(DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ' Uchumu kwa Ajira na Biashara
Endelevu' yanayofanyika katika Viwanja vya Julius Nyerere Temeke jijini
Dar es Salaam.
Mashiba alisema UCSAF imejipanga katika
kuhakikisha huduma za mawasiliano na mtandao zinafikia Watanzania wote
kwa miaka mitano ijayo hivyo wanaendelea kuwezesha wadau ili kufikia
lengo hilo.
Alisema kiasi hicho cha shilingi bilioni 32
zitatekeleza miradi mbalimbali hasa vijijini na mipakani ambapo huduma
ya mawasiliano ina changamoto.
“Jukumu la kupeleka huduma ya
mawasiliano tunalitekeleza kwa kushirikiana na kampuni zilizopewa lesini
na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ili kuhakikisha watu wa
kijijini kama Narung’ombe na mipakani kunapata utatuzi wa huduma hiyo
muhimu kwa maendeleo na uchumi wa nchi,” alisema.
Alisema hii ni
mara ya pili wao kushiriki Maonesho ya Sabasaba ambapo wametembelewa na
wageni zaidi ya 500 lakini ageni 63 wameelezea changamoto ya mawasiliano
hasa vijijini hivyo kupitia changamoto hizo watahakikisha huduma za
mawasiliano zinapatikana.
Mashiba alisema pia watahakikisha
wanatatua changamoto ya maeneo ya mipakani kusikiliza redio za nje
ambapo watawezesha vyombo vya habari kuwa na uwezo wa kufika huko.
Aidha,
alisema wanatarajia kutoa komputa 800 kwa shule ambapo kila shule
itapatiwa komputa tano na mashine ya kuprinti moja lengo likiwa ni
kurahisisha huduma za TEHAMA kwa walimu na shule.
Mkurugenzi huyo
alisema UCSAF ipo tayari kuwezesha kada zote ambazo zinachangia
upatikaji wa huduma ya mawasiliano kupatikana kwa urahisi.
Akizungumzia
mipango hiyo ya UCSAF Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,
Dk. Faustine Ndugulile alisema changamoto hizo za mwasiliano pembezoni
na katika wilaya kumi ambazo bado zina changamoto zitataliwa mwaka huu
wa fedha.
Ndugulile alisema kwa kuanzia UCSAF imewezesha usikivu wa redio ya TBC ambapo studio ya Dodoma na Arusha zimeboreshwa.
Alisema
mikakati ya wizara yake kwa kushirikiana na UCSAF ni kuleta mapinduzi
katika kada ya mawasiliano ili kuchangia ukuaji wa uchumi na maendeleo.
No comments:
Post a Comment