Mkurugenzi wa Kampuni ya Chocolate Princess Mboni Masimba akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza rasmi Usiku waTamasha la Vyakale Dhahabu litakalofanyika Disemba 10 mwaka huu.
Mkongwe wa Taarab nchini Afua Suleiman  akitoa pongezi kwa Muandaaji wa Tamasha Hilo Mboni Masimba kwa kuandaa Tamasha Hilo lenye Lengo la kuwapa Burudani wapenzi wa Taarabu.
Malkia wa Taarabu nchini Khadija Kopa akizungumza kuhusu Tamasha la vya Kale dhahabu akiwataka wapenzi wa Muziki wa Taarab kujitokeza kwa wingi huku wakivalia Mavazi ya heshima
Malkia wa Taarabu nchini Khadija Kopa akizungumza kuhusu Tamasha la vya Kale dhahabu akiwataka wapenzi wa Muziki wa Taarab kujitokeza kwa wingi huku wakivalia Mavazi ya heshima
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
Rais
 Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa Usiku wa 
Tamasha la Vyakale Dhahabu utakaofanyika Disemba 10 mwaka huu katika 
UKumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
 na wanahabari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kampuni ya 
Chocolate Princess ambaye pia ni Muandaji wa tamasha hilo Mboni Masimba 
amesema usiku huo utafanyika lengo likiwa kusherehekea Miaka 60 ya Uhuru
 wa Tanzania.  
" Tamasha hili ni la taarabu 
asilimia 100  tunakwenda kulitumia kusherehekea miaka ya 60 ya uhuru pia
 kuwaenzi wakongwe wa muziki wa taarabu hivyo litakaonga nyoyo za 
wapenzi wa muziki wa mwambao," amesema.
Amebainisha
 kuwa usiku huo utafanyika kwa ajili ya kuwaenzi wakongwe wa muziki huo 
akiwemo Issa Matona na Bi Kidude, hivyo Rais wa Awamu ya Nne Dkt. 
Kikwete atakuwa mgeni rasmi.
Amewataja waimbaji
 watakaosindikiza usiku huo ni Khadija Kopa, Patricia Hilary, Afua 
Suleiman, Sabaha Muchacho, Khadija Yusuf, Mzee Yusuf, Abdul Misambano, 
Ally Star na wengine wengi.
Ameongeza kuwa 
kiingilio cha tamasha hilo ni Sh elfu 50 ikijumuisha chakula na vinywaji
 na kwamba wanaume na wanawake wameshauriwa kuvalia mavazi ya Pwani.
Kwa
 upande wake, Muimbaji Mkongwe wa Taarabu, Khadija Kopa amempongeza 
Mboni kwa kuandaa tamasha hilo huku akiwasisitiza wapenzi wa muziki huo 
kujitokeza kwa wingi kupata burudani.
Nae, 
Mmoja wa Wadhamini wa Usiku huo ambaye pia ni Meneja Masoko wa Kampuni 
ya K4s Security, Bico Scanda amesema wanayo furaha kuwa sehemu ya 
tamasha hilo na kuwahakikishia wapenzi wa muziki huo watakuwa  salama na
 mali zao wakiwa ukumbini humo.
 
 
 
 

 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment