Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya CRDB, Mshindo Magimba (katikati) na balozi wa CRDB, Frida Amani (kulia), wakiangalia namba ya mteja wa benki hiyo wakati wa uchezeshaji wa droo ya kumtafuta mshindi wa gari jipya aina ya IST kwa wateja wanaotumia SimBanking. Droo hiyo ilifanyika Oktoba 17, 2025 jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja wa Huduma za Benki Kupitia Simu ya Mkononi wa CRDB, Amina Mawona.
Meneja wa Huduma za Benki Kupitia Simu ya Mkononi wa Benki ya CRDB, Amina Mawona (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya kumtangaza mshindi wa gari aina ya IST, anayetumia huduma ya SimBanking ya CRDB, jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa benki hiyo, Mshindo Magimba na kulia ni Balozi wa CRDB, Frida Amani.


No comments:
Post a Comment