Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi Geofrey Mkinga akizungumza katika kikao hicho na kueleza kuwa mabadiliko yaliyofanywa na Serikali kwa kushirikiana na wakala huyo yana tija kwa wananchi wa hali ya chini.
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam
WAKALA
wa Barabara za Vijijini na Mjijini Tanzania (TARURA) imetoa elimu ya
kuwajengea uwezo Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na Kamati ya
Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ilala juu ya matumizi ya Mfumo wa
Kieletroniki wa Ushuru wa Maegesho (TeRMIS) ambao utaanza kutumika tena
Disemba Mosi mwaka huu katika mikoa ya Dar es Salaam, Iringa, Mwanza,
Singida na Dodoma.
Akifungua
kikao hicho jijini humo Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Charangwa
Makwiro amesema mfumo huo wa ukusanyaji mapato ni sahihi katika kuzuia
mapato yaliyokuwa yanapotea pamoja na kuziba mianya mbalimbali
iliyosababisha kupotea kwa mapato hayo.
Amebainisha,
kushirikishwa kwa Madiwani na viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama
wa jiji hilo ni muhimu kwa kuwa hao ni viungo muhimu walio karibu na
wananchi hivyo wanategemea matokeo chanya mara baada ya mkutano huo
katika uwezeshaji wa kufanikiwa kwa mfumo huo.
Kwa
upande wake, Meneja wa TARURA Mkoa wa Dar es Salaam Mhandisi, Geofrey
Mkinga amesema matumizi ya mfumo huo ni katika kwenda na azma ya
Serikali ya kuhama kutoka mfumo wa analojia kwenda kidigitali hasa
katika ukusanyaji wa mapato na baada ya changamoto kadhaa kutokea na
kusimamishwa kwa mfumo huo kwa muda marekebisho yamefanyika na elimu
zaidi imetolewa kwa Umma kupitia makundi mbalimbali yakiwemo vongozi na
waandishi wa habari ili wananchi waweze kufikiwa na taarifa hizo na
kwenda sambamba na mfumo huo wa ukusanyaji mapato.
Kuhusiana
na mabadiliko yaliyofanyiwa kazi ni pamoja na kupunguzwa kwa adhabu ya
30,000 na adhabu ya mara mbili ya kutofanya malipo baada ya siku saba na
kuongezwa kwa siku 14 za malipo na ndani ya siku hizo mteja
atakumbushwa mara mbili huku watumiaji wa mitandao ya simu
wakikumbushwa kufanya malipo na kampuni hiyo.
Mhandisi
Mkinga amesisitiza kuwa mabadiliko hayo yamepunguza tozo ya siku kutoka
shilingi 4500 hadi 2500 na tozo kwa saa ikibaki Sh 500 huku taarifa za
wapi mteja alipaki zitabaki kuwa siri kwa usalama wa mfumo na watumiaji
wake.
Nae,Meneja
wa TEHAMA kutoka TARURA, Stanley Mlula amesema wamebadilisha mfumo wa
ulipaji tozo zitabaki kama zilivyo na hiyo ni kwa malengo ya kuzuia
kupotea kwa mapato kwa kuzuia malipo ya fedha mbichi (cash) na kutumia
mfumo wa malipo ya 'control number' ambapo wateja watalipa kwa simu na
benki (NMB na CRDB.)
Mstahiki
Meya wa Jiji hilo, Omary Kumbilamoto ameipongeza TARURA kwa kupitia
changamoto hizo kwa kushirikiana na Serikali (TAMISEMI) na wanaamini
mfumo huo utafanya kazi kwa mafanikio makubwa hasa katika ukusanyaji wa
mapato.
Meya
Kumbilamoto amefafanua kuwa ni muhimu kwa Wakala hiyo kuwashirikisha
madiwani na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama katika masuala
yanayohusu jamii kutokana na muunganiko muhimu na wa moja kwa moja wa
viongozi hao na wananchi.
No comments:
Post a Comment