HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 13, 2022

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZIKO YA MKE WA MWANDISHI WA HABARI TALIB USSI



Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,  Alhaj  Othman Masoud Othman, akimpa pole leo Mwandishi wa Habari Talib Ussi Hamad kwa kufiwa na Mke wake Marehemu Bi. Hafsa Said Salum, Septemba 11, 2022.




Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,  Mheshimiwa Alhaj  Othman Masoud Othman, leo Septemba 12, 2022 amejumuika na Wananchi na viongozi mbali mbali wa Kiserikali, Dini na Kisiasa  katika Maziko ya Marehemu Bi. Hafsa Said Salum, Mke wa Bw.Talib Ussi Hamad (Mwandishi wa Habari).

Marehemu Bi. Hafsa aliyefariki dunia jana Septemba 11, amezikwa katika Makaburi ya Kianga, Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.
 
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Peponi, Amin!

No comments:

Post a Comment

Pages