HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 22, 2023

GWAJIMA ANOGESHA UFUNGUZI LADIES FIRST DIMBA LA BENJAMIN MKAPA, DAR


Waziri Dk. Dorothy Gwajima, akizungumza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Riadha ya Ladies First.

 Kaimu Katibu Mkuu RT, Wakili Jackson Ndaweka, akitoa salamu za shirikisho. 

 Viongozi wa RT, Makamu wa Rais William Kallaghe, Kaimu Katibu Mkuu Wakili Jackson Ndaweka na Mwanariadha Simbu, waliosimama nyuma wakiwa katika picha ya pamoja na meza kuu, wakati wa ufunguzi Ladies First.

Waziri Dr. Gwajima, wa pili kutoka Julia akishiriki mazoezi ya viungo wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Ladies First. Wa kwanza kutoka kulia ni Mwenyekiti BMT, Leodegar Tenga, Balozi wa Japan Tanzania kushoto kwa Waziri na Katibu Mtendaji BMT, Neema Msitha.

 

NA TULLO CHAMBO

MSIMU wa Nne wa Mashindano ya Riadha ya Wanawake maarufu kama 'Ladies First' umefunguliwa kwa kishindo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam Januari 21 na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dr. Dorothy  Gwajima.

Mashindano hayo  ya siku mbili yameandaliwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), kwa kushirikiana na  Shirikisho la Riadha Tanzania (RT).
 
Ufunguzi huo, ulipambwa na vikundi mbalimbali vya Joging, burudani mbalimbali akiwamo Msanii maarufu wa Singeli, Dullah Makabila, aliyepagawisha vilivyo na wanariadha wa kike

Akizungumza katika uzinduzi huo, Dr. Gwajima, alisema wataend…
[10:45 PM, 1/21/2023] Tullo Vd: Mashindano hayo, RT, vyama vya Riadha vya Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa kwa kuwezesha wachezaji wao kufika Dar Ed Salaam kwa ajili ya mashindano hayo, Ofisi ya Mkurugenzi Manispaa ya Temeke kwa kuruhusu zaidi ya wanafunzi 1,000 kuhudhuria mashindano hayo na kujifunza, na Mwanariadha mahiri wa zamani, Kanali Mstaafu Juma Ikangaa, ambaye pia ni Balozi wa Hiari wa JICA, kwa kuasisi wazo la kuanzishwa mashindano hayo.

Balozi mwingine wa hiari wa JICA, Mwanariadha mshindi wa medali ya Fedha Jumuiya ya Madola, Alpohonce  Simbu, aliwataka wanariadha wa kike hao watumie fursa hiyo kujituma na kurejesha enzi za Mwanamama Theresia Dismas, ambaye ni mchezaji wa kwanza kuipa Tanzania medali ya kimataifa katika michuano ya All African Games 1965.

Simbu, alisema kuwa ushiriki huo utakuwa chachu ya kujifikiria namna ya  Theresia Dismas alieweza kupata medali.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mkuu RT, Wakili Jackson Ndaweka, aliishukuru Serikali kwa kuwezesha kupata muungano na JICA kwa kudhamini Riadha hususani kwa wanawake.

Àlisema kuwa wanawake wanatakiwa kutumia fursa ya kujiendeleza  ,kwani mahitaji kuleta ushindani .

Mashindank hayo yatakayofikia tamati Januari 22, yanashirikisha wanariadha zaidi ya 186 kutoka mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani.

Uzinduzi huo, pia ulihudhuriwa na Balozi wa Japan nchini Tanzania, viongozi kutoka Wizara ya Michezo Sudan Kusini, Naibu Meya Jiji la Nagai Japan, Mwenyekiti wa BMT Leodegar Chilla Tenga na Makamu wa Rais RT, William Kallaghe.

No comments:

Post a Comment

Pages