HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 20, 2023

NATALIA, SULLE KUSHIRIKI CROSS COUNTRY KENYA

WANARIADHA wawili wa Tanzania, Natalia Elisante na Herman Sulle, wanatarajia kushiriki Mashindano ya Taifa ya Mbio za Nyika Kenya 'Kenya National Cross Country' kwa upande wa Senior.

Mashindano hayo, yanatarajiwa kufanyika jijini Nairobi Januari 21, kwenye viwanja vya Chuo cha Magereza Ruiru.


Kwa mujibu wa Kaimu Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Wakili Jackson Ndaweka, wanariadha hao, wamepata hiyo baada ya RT kupokea mwaliko kutoka kwa wenzao wa Kenya (AK).


Katika mashindano hayo, mshindi wa kwanza atajipatia Dola 1000 za Marekani zaidi ya Sh. Milioni 2 za Tanzania.


Mshindi wa pili Dola 800 huku wa tatu akiondoka na dola 700 ambapo hadi mshindi wa 12 atapata zawadi ya fedha.


Nchi mbalimbali ikiwamo Tanzania, hivi sasa zinajiandaa na mashindano ya Nyika ya Dunia yanayotarajiwa kufanyika nchini Australia February 18 mwaka huu.


Timu ya Tanzania, inatarajiwa kuingia kambini Februari Mosi jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Pages