HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 11, 2023

MAKAMU MWENYEKITI TWCC AHIMIZA TUTHAMINI BIDHAA ZA NDANI


Mkurugenzi wa TWCC Mwanaidi hamza akizunguma na wajasiriamali hawapo pichani  kwenye Ukumbi wa Mikutano Mlimani City Jijini Dares es Salaam.

 

Na Khadija Kalili


MAKAMU MWENYEKITI wa  Chama  cha  Wanawake  Wafanyabiashara  Tanzania (TWCC) Victoria Mwanukuzi  ametoa wito  kwa watanzania wote kuthamini na kununua bidhaa za ndani kwani ndiyo njia kubwa ya kuweza kuzipandosha thamani na kukuza uchumi wa wajasiriamali na wafanyabiashara  kwa ujumla.

Makamu Mwenyekiti Mwanukuzi amesema hayo leo Machi 10 alipokua mgeni rasmi alipozungumza kwenye kongamano la wajasiriamali na wafanyabiashara wanawake kwenye Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar Es  Salaam.


 "Tumekutana leo ikiwa ni latika muendelezo wa kusherehekea siku ya Mwanamke Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Machi nane ambapo sisi tumeiita siku ya wajasiriamali wa Afrika   bado tunaendelea kusherehekea pamoja hivyo nawasisitiza tupende kununua bidhaa za nyumbani kwa sababu zina ubora madhubuti kushinda hata hizo bidhaa za nje kwa sababu sisi bidhaa zetu ni za asili" amesema.


"Tuhamasishane kupenda vya nyumbani mimi binafsi nikiingia kufanya manunuzi  kwenye maduka makubwa 'Super Market' huwa nanunua bidhaa zilizoandikwa Made in Tanzania yote hii ni kwa sababu ya kuwa na uzalendo" amesema Mwanukuzi.


Mhandisi Lightness Salema ambaye pia ni miongoni mwa wajasiriamali amesema kuwa wakati umefika kwa mjasiriamali ili anyanyukelazima ajinyanyue mwenyewe ndipo atainuliwa   na kusogezwa huku akisisitiza  lazima mwanamke awe mwaminifu kwenye biashara kwa ujumla ikiwa ni pamoja na kuweka taarifa za biashara zake.


Mkurugeni wa TWCC Mwajuma Hamza  amesisitiza kuwa hivi sasa tunaelekea katika soko huru la Afrika  hivyo wajasiriamali ni wajibu wao kujituma.na kujikuza ili kuweza kukabiliana na ushindani wa biashara wakati utakapo fika licha ya kuwa wanakabiana na changamoto mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Pages