Na Jasmine Shamwepu, Dodoma
Shirika
la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), imebainisha kuwa inatekeleza
miongozo inayotolewa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) katika
kuhakikisha manunuzi, matumizi bora, sahihi na salama ya vifaa na mifumo
yote ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Serikalini
yanazingatiwa.
Hayo
yameelezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Kaimu Abdi Mkeyenge leo
Jijini Dodoma, wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya
TASAC, pamoja na kubainisha Mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha
miaka miwili ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita.
Mkeyenge
amesema kuwa TASAC imeunganisha ofisi zake zote zikiwemo zile za Mikoa,
Wilaya na mipakani kwenye Mkongo wa Taifa ambao umerahisisha na
kuharakisha mawasiliano ya ndani (Intranet), barua pepe, na mawasiliano
na wadau wa nje .
Aidha
,Mkeyenge ameongeza kuwa uendelezaji wa miundombinu na mifumo ya TEHAMA
ulianza mwaka wa fedha 2018/19 na utakamilika mwaka wa fedha 2025/26
huku mifumo ambayo inayoboreshwa ndani ya Shirika ni pamoja na mfumo wa
ukaguzi, usajili wa vyombo vya usafiri kwa njia ya maji na utoaji wa
vyeti vya Mabaharia (Maritime Administration Management System), mfumo
wa utoaji leseni, ukusanyaji wa mapato ya udhibiti, uhakiki kadhia na
kutoa ankara za malipo ya watoa huduma wa meli (Manifest Billing
System), pamoja na mfumo wa kutoa huduma za biashara ya Meli.
Mamlaka
ya Serikali Mtandao (eGA) imetusaidia katika kuhakikisha manunuzi,
matumizi bora, sahihi na salama ya vifaa na mifumo yote ya Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Serikalini tunaitumia kwa mafanikio
makubwa na tunaami mpaka mwaka wa fedha wa 2025/26 mifumo yote ndani ya
Shirika itakuwa tayari,"
Pia
Mkeyenge amesema katika kuimarisha usimamizi wa usalama, ulinzi na
utunzaji wa mazingira dhidi ya shughuli za meli na kupunguza matukio ya
ajali za vyombo vya majini TASAC imefanya sensa na kaguzi za vyombo vya
usafiri majini ambapo kaguzi 6,208 katika mwaka wa fedha 2021/22
zilifanyika na kaguzi 4,490 zilfanyika katika kipindi cha Julai 2022
mpaka Januari 2023 inayotarajiwa kufikia vyombo takriban 8,000 ifikapo
mwezi Juni 2023.
No comments:
Post a Comment