HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 06, 2023

Milioni 20 za mfuko wa jimbo la Kibaha Mjini zaleta neema ya miradi kwa wananchi

 Na Victor Masangu, Kibaha


Katika kuchagiza chachu ya kuleta  maendeleo kwa wananchi mfuko wa Jimbo kutoka ofisi ya Mbunge wa Kibaha mjini imeamua kutoa zaidi ya kiasi cha shilingi milioni 20 katika kusaidia kuinua na kuchochea kasi ya maendeleo katika sekta mbali mbali.


Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvesty Koka wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuweza kukagua na kutembelea baadhi ya miradi ambayo inatekelezwa kupitia fedha za mfuko wa Jimbo.

Ziara hiyo ambayo iliambatana na wajumbe mbali mbali wa mfuko wa Jimbo pamoja na viongozi wengine wa Chama Cha mapinduzi (CCM) ngazi za matawi,mashina,kata,pamoja na wilaya ili kuweza kujiridhisha kama miradi hiyo inafanyika kwa kiwango kinachotakiwa 

Akizungumza pindi alipokuwa katika miradi hiyo Koka alisema kwamba katika fedha hizo ambazo zilishatolewa ni kwa ajili ya kuchochea zaidi kasi ya maendeleo katika miradi mbali mbali ikiwemo,afya,elimu,miundombinu ya barabara maji na huduma nyingine za kijamii.

Aidha Mbunge huyo alifafanua kwamba katika fedha hizo zimeweza kusaidia mambo mbali mbali ikiwemo ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za msingi na sekondari,ununuzi wa madawati na viti katika shule mpya ya sekondari Misugusugu.


Pia aliongeza kuwa katika fedha hizo zimeweza kutumika katika kuanzisha mradi wa ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika kata ya Mbwawa kwa lengo la kuwasaidia wakinamama wajawazito kuondokana na changamoto ya kutwmbea umbari mrefu kufuata huduma ya kujifungulia.

Sambamba na hilo alifafanua kuwa dhamira yake kubwa ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa pamoja na hususan atazipa kipaumbele kwa Hali na mali kata ambazo zipo pembezoni mwa mji.

"Mimi Kama Mbunge lazima niweke mipango madhubuti ya kushirikiana na wananchi na ndio maana nimeamua kutumia fedha hizi za mfuko wa Jimbo ili kuchochea kasi ya maendeleo na mieanza ziara yangu katika kata zipatazo sita na nitamalizia na nyingine kwani Jimbo langu lina kata 14,"alisema Koka.

Nao baadhi ya wananchi ambao wamenufaika miradi hiyo ambayo imetokana  na fedha za mfuko wa Jimbo wameishukuru serikali ya awamu ya sita pamoja na Mbunge Koka kwa kujikita zaidi katika kuwaletea maendeleo yenye tija kwa maslahi ya jamii kwa ujumla.

Fedha za mfuko wa jimbo zimekuwa zikitolewa kwa ajili ya kuweza kuchochea maendeleo kupitia miradi mbali mbali ikiwemo afya,elimu,maji,umeme,miundombinu ya barabara,pamoja na huduma nyingine za kijamii.


Ziara hiyo ya Mbunge wa Jimbo a Kibaha mjini ya kutembelea miradi yamaendeleo imefanyikakatika kata sita ikiwemo Mbwawa, Visiga, Misugusugu, Viziwaziwa, Kibaha, pamoja na kata ya mkuza.
 
Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini akiwa na viongozi wa CCM pamoja na wajumbe wa mfuko wa Jimbo wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo.

No comments:

Post a Comment

Pages