HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 29, 2023

MKE WA MBUNGE KIBAHA MJINI MAMA SELINA KOKA AAHIDI KUFANYA HARAMBEE YA UJENZI WA MADARASA SHULE YA MSINGI KAMBARAGE

 


Kutoka kushoto Diwani wa Viti Maalumu Chama Cha Mapinduzi (CCM) Lidya Mgaya anayefuata Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mama Selina Koka akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage Happiness Msaki na  Mjumbe Kamati ya Siasa Catherine Katele (Mwenye Suti) wengine wanaoshuhudia ni Diwani Kata  ya Tumbi Kibaha Raymond Chokala  na Asha Baraka.


Na Khadija Kalili


MKE wa Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mkoani Pwani Bi Selina Koka ameahidi kuandaa harambee maalumu  itakayochangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa  nane ikiwa ni katika kutatua changamoto  za upungufu wa madarasa  Shuleni  hapo.

Mama Koka amesema hayo leo  Mei  29 asubuhi  alipofika Shuleni  hapo kwa ziara maalumu na kuweza kujionea hali halisi jinsi ilivyo huku akiwa ameambatana na Viongozi mbalimbali  wakiwemo Diwani  wa Kata ya Tumbi Mheshimiwa  Raymond  Chokala,Mjumbe Kamati ya Siasa Catherine  Katele na wadau wengine mbalimbali  wa masuala ya Siasa akiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) ,MNEC Mstaafu Asha Baraka.


Mama Koka ameshiriki katika uchangiaji mpango wa kunywa uji Shuleni   hapo ambapo pia ametoa sukari mifuko 20 kwa ajili ya wanafunzi wa  darasa la awali na darasa la kwanza pia ametoa  katuni 180 ambazo waligaiwa wanafunzi wa darasa la kwanza shuleni hapo.


Akizungunzia kuhusu harambee hiyo Mama Koka amesemakuwa wataunda Kamati maalumu ambayo itaratibu namba ya uchangi

shaji wa fedha za ujenzi wa madarasa ambayo yatakwenda sanjari na ukarabati wa madarasa yaliyochakaa huku yeye ameahidi kukarabati darasa la wanafunzi wa darasa  la awali.

Aidha Mama Koka  amesema kuwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini ameahidi kununua madawati 70 kati ya 140 ambayo yanahitajika shuleni hapo.

"Wakati huohuo Mke wa Mbunge huyo ametoa wito kwa wazazi wa wanafunzi hao kujijengea mioyo ya kuchangia masuaala mbalimbali  ambayo yataleta maendeleo katika Shule  huku akiwaambia msirudi kwenye uchangiaji  mkisikia kuna michango ya 1,000 au 2,000 changieni ili na sisi tukija pamoja na Viongozi  wengine na kuona mwamko wenu katika uchangiaji mnatupa moyo zaid i wa kujitolea" amesema Mama Koka.


Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kambarage Happines Msaki amesema kuwa shule hiyo inachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja na kukosa uzio jambo ambalo huchangia kukosesha usikivu kwa wanafunzi shuleni hapo.

Wakati huohuo  Mheshimiwa  Diwani wa Kata ya Tumbi  Kibaha  Mkoani Pwani  ameongea kwa uchungu madhila yanayowakuta baadhi ya wanafunzi Shuleni  hapo "Nawaomba wazazi muwe walinzi wa wanafunzi hawa ambao ni watoto wetu jambo hili la ukosefu  wa maadili nalizungumza kwa uchungu mwingi,suala la ukatili wa kijinsia katika Kata hii ya Tumbi Shule hii tunaongoza   kwa vitendo hivi viovu kwani kuna kesi 20 na nyingi ni za shuleni hapa ,hivyo nauomba uongozi wa Shule tushirikiane pamoja katika haya mapambano na sisi Viongozi wa Kata ya Tumbi tumejipanga vizuri na hizo kesi ambazo tayari ziko Polisi tunazifuatilia  kwa ukaribu wa hali ya juu si sahihi kuwaharibia watoto  maisha hii ni dhambi  kubwa huku watendaji wa vitendo hivyo wakiwalaghai kwa kuwapa chip's, chocolate  na kuwabaka hili jambo halikubaliki"amesena Diwani   huyo wa Tumbi Chokala.

No comments:

Post a Comment

Pages