HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 29, 2023

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2bn/-

 

Afisa Mkuu wa wateja Wakubwa na Serikali wa NMB, Alfred Shayo (kushoto) akikabidhi hundi ya shilingi milioni 200 iliyotolewa kwa ajili ya udhamini wa Mkutano wa 37 wa ALAT unaofanyika Arusha. Anayepokea hundi ni  Makamu Mwenyekiti wa ALAT, Sima Constatin na wengine ni baadhi ya maafisa waandamizi wa Benk ya NMB na pia kutoka ALAT. Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Praygod Mphuru (wa pili kushoto), Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali wa NMB,Vicky Bishubo (wa tatu kushoto) Mkurugenzi wa Halmashauri ya Geita, Zahara Michuzi na Katibu wa ALAT Taifa, Mohamed Maje (wa pili kulia). (Na Mpiga Picha Wetu).

 


Na Mwandishi Wetu


Benki ya NMB imebainisha utayari wake wa kuendelea kufanya kazi kwa karibu na serikali za tawala za mitaa, ikiwemo kufadhili mikutano ya kila mwaka ya Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT).

 
Dhamira ya kudumisha ushirikiano huo iliwekwa bayana jana jijini Arusha na benki hiyo wakati inatangaza ufadhili wa TZS milioni 200 wa mkutano mkuu wa 37 wa ALAT ambao umeanza rasmi leo hii.

 
Wakizungumza kabla ya kutangazwa kwa udhamani wa mwaka huu kwenye Ukumbi wa AICC, viongozi waandamizi wa NMB walisema hii ni mara ya saba kwa taasisi yao kufanya hivyo.

 
Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa na Serikali, Bw Alfrded Shao, alisema udhamini walioufanya ndani ya kipind hicho sasa umefikia zaidi ya TZS bilioni 1.2.


“Tuna miaka zaidi ya saba pamoja na ALAT katika masuala ya maendeleo ya taifa letu na ndio maana wenzetu walipotufuata tuwaunge mkono hatukusita hata kidogo,” alibainisha.


“Hata hivyo, kubwa zaidi leo tunatangaza ushiriki wetu kama mdhamini wa Mkutano Mkuu wa ALAT kwa kiasi cha TZS milioni. 200 ilikufanikisha mkutano huu,” aliongeza na kusema wamekuwa wakishirikiana na ALAT hasa kusaidia kuboresha miundombinu ya elimu, afya, usafiri na mazingira kupitia wananchama wake ambao ni halmashauri 184 nchini kote.

 
Aidha, Bw Shao aliitumia hafla ya kukabidhi hundi ya udhamani wa mwaka huu kuonyesha jinsi NMB inavyozihudumia halmashauri, serikali kuu na taifa kwa ujumla hasa kupita huduma zake bunifu za kifedha.


Alisema moja ya maeneo ambayo wamefanikiwa katika hilo ni kurahisisha ukusanyanji wa kodi kupitia mifumo bora inayowezesha Serikali ya Awamu ya Sita katika kukusanya mapato yake.


“Ubunifu na uwekezaji ambao tumeufanya kwenye teknolojia ulituwezesha kuwa benki ya kwanza kuunga mifumo yetu na Mfumo wa Kielektroniki wa Malipo ya Serikali (GePG) na hadi sasa zaidi ya taasisi 1,100 tayari zimeunga mifumo yake kwenye mifumo ya NMB ya ukusanyaji wa mapato,” kiongozi huyu alibainisha.


“Kwa mfano, kupitia mifumo yetu mbalimbali ya malipo tumewezesha Serikali kukusanya TZS trilioni 8.6 kupitia GePG kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2019 hadi 2021,” aliongeza kusema akisisitiza kuwa fedha hizi zilikusanywa kupitia mifumo ya kidijitali kama NMB Mkononi, NMB Wakala na hata internet banking.

 
Kauli mbiu ya mkutano mkuu wa ALAT wa mwaka huu ambao ni wa siku tatu ni: “Uboreshaji wa Miundombinu ni Chachu ya Utoaji wa Huduma Bora katika Mamlaka za Serikali za Mitaa”.

 
Makamu Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Bw Sima Costantine Sima, aliipongeza NMB kwa kusaidia kuboresha upatikanaji wa huduma hasa zile za kifedha nchoni lakini pia mchango wake katika kuendeleza ustawi wa jamii.


Alisema ALAT na wananchama wake 184 wanathamini ushirikiano wao mzuri wa kibiashara na kimaendeleo na benkii hiyo ambao umekuwa ni wa manufaa kwa wao wote pamoja na wananchi wanaowahudumia.

No comments:

Post a Comment

Pages