HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 31, 2023

VIJANA KAGERA WATARAJIA KUNUFAIKA NA UFUGAJI KUPITIA RANCHI ZA SERIKALI

Na Lydia Lugakila, Bukoba


Vijana Mkoani Kagera wanatarajia kujikwamua kiuchumi kupitia fursa ya ufugaji wa kisasa na wa kistaarabu utakaofanyika kupitia katika Ranchi za Serikali zilizopo Mkoani humo.

Kauli hiyo imebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Bi Fatma Mwassa katika kikao na Viongozi wa dini Manispaa ya Bukoba  kilichofanyika katika ukumbi wa Mkoa huo.


Bi Fatma amesema Mkoa huo una Ranchi nyingi za Serikali ambazo watu wanaweza kufuga kisasa na kistaarabu na kuwa kwa sasa Ranchi nyingi kati ya hizo hazijaanza kutumika.


"Tutatengeneza vizuri  utaratibu ili kutoa Fursa kwa Vijana kufuga Ng'ombe ili wanufaike  na biashara hiyo hivyo ni jukumu letu Sisi kama Serikali kuwasaidia Vijana wapate mitaji ya Ng'ombe" alisema Bi Fatma.


Ameongeza kuwa changamoto iliyopo nikwamba bado Vijana hawajaandaliwa vizuri kuijua fursa hiyo Ila ana imani wataitambua fursa hiyo kwa haraka jambo litakalo saidia katika kuunyanyua Mkoa huo kuichumi.

No comments:

Post a Comment

Pages