Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (katikati), akizungumza wakati alipokuwa akiukagua mradi wa maji katika Kijiji cha Matare uliotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Ikungi wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Juni 6, 2023.
......................................................
Na Dotto Mwaibale, Ikungi
MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba
amefurahishwa na kuridhishwa na usimamizi mzuri na ukamilishaji wa
miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi na kuwapongeza
viongozi wote kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwa thamani halisi ya fedha zilizotolewa
na Serikali.
Serukamba ametoa pongezi hizo wakati
wa ziara yake wilayani humo aliyoifanya leo Juni 6, 2023 ambapo alipata fursa
ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuhimiza ikamilike
kabla ya Julai 1, 2023.
Aidha, Serukamba amewapongeza wataalam na wananchi kwa kuunga mkono juhudi
za serikali kwa kuchangia utalaam na nguvu kazi katika kutekeleza miradi hiyo
ambayo imegharimu fedha nyingi.
"Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa kwa
kutoa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi hii naomba tumuheshimishe
Rais wetu kwa kuikamilisha haraka kabla ya Julai 1, 2023 ili ianze
kutumika," alisema Serukamba.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi imekuwa ikimpa raha kutokana na
kufanya vizuri katika kutekeleza miradi ya maendeleo na kuwa imekuwa ikipata
mafanikio hayo kutokana na ushirikiano uliopo baina ya viongozi, wataalam na
wananchi.
Miradi aliyoitembelea na kuikagua ni mradi wa maji katika Kijiji cha Matare
uliopo Kata ya Unyahati uliogharimu Sh. Milioni 386.8 ambao utawahudumia
wananchi 5036, ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Matare na ujenzi wa
mabweni mawili na bwalo katika Shule ya Msingi
Ikungi.
No comments:
Post a Comment