HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 23, 2023

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YAWAFUNDA WANAHABARI RUVUMA KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID

 NA STEPHANO MANGO, SONGEA

 
WAZIRI wa Katiba na Sheria  ambaye pia ni Mbunge  wa Jimbo la Songea Mjini Dkt.Damas Ndumbaro amewataka waandishi wa Habari hapa Nchini  kupambana na mifumo kandamizi ya ukatili wa kijinsia na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha  wanafanya uendelevu wa kuibua,kuandika na kuripoti taarifa za matukio ya vitendo vya ukatili Kwa jamii.


Dkt Ndumbaro ameyasema hayo  jana Mjini hapa wakati akizungumza na waandishi wa Habari 25 kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma wanaoshiriki warsha ya siku mbili kuhusu ukatili wa kijinsia Kwa vyombo vya Habari inafanyika katika Hotel ya Heritage Cottage. 


Dkt Ndumbaro alisema kuwa washiriki wa mafunzo haya wanatakiwa kuandika na kuibua vitendo vya ukatili wa Kijinsia na kwamba kwa waandishi  3  watakaofanya vizuri katika uandishi wa Taarifa anuai watapata zawadi mbalimbali

Alisema kuwa katika kuelekea Uzinduzi wa kampeni ya Mama Samia Legal Aid itakayofanyika Julai 22 katika uwanja wa Majimaji Mjini Songea Mkoani Ruvuma ,na baada ya uzinduzi huo utoaji elimu utaendelea Kwa muda wa siku 10, hivyo Waandishi wanatakiwa kuhabarisha Umma juu ya Kampeni hiyo

Alieleza kuwa Waandishi watatu ambayo watakaoshinda kuripoti vizuri taarifa hizo Wizara ya Katiba na Sheria itawazawadia fursa mbalimbali  ikiwemo fedha taslimu ,Medali pamoja na kupata nafasi ya kuwa Balozi wa kupinga ukatili wa Kijinsia Kwa wananchi,na pia Balozi huyo atapata fursa ya kwenda Kwenye mikoa mbalimbali hapa Nchini  akiwa ameambatana na maafisa wa Wizara ya Katiba na Sheria. 

Warsha hiyo ya siku mbili imefadhiliwa na Serikali kupitia  wizara ya Katiba na Sheria,na mwezeshaji  wa warsha hii  ya ukatili wa kijinsia ni Dkt. George Chambua ambaye  ni  Mbobezi wa masuala ya GBV.

Kwa upande wake Mratibu wa Mafunzo hayo George Mollel ameitaja Kampeni ya Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kuwa inalenga kulinda na kukuza haki ya upatikanaji haki kupitia huduma za msaada wa kisheria nchini

Mollel alisema kuwa kampeni inatarajia kuboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza hususan wanawake,Watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu,kampeni itachangia kuimarisha amani na utulivu na kuleta utengamano wa kitaifa

Alisema kuwa elimu ya kisheria italenga katika masuala ya ukatili wa kijinsia,migogoro ya ardhi,mirathi,usuluhishi kwa njia  mbadala,mifumo ya kisheria na masuala yahusuyo haki za binadamu kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Pages