HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 01, 2023

KAMPUNI YA ASAS YAPONGEZWA


Mkuu wa wilaya Mufindi, Dk. Linda Salekwa akikabidhi Kajuna Maurice zawadi ya bingwa wa mashindano ya gofu ya wazi ya Mufindi 2023

 

NA DENIS  MLOWE, MUFINDI


MKUU wa wilaya ya Mufindi Dr.Linda Salekwa  ametoa pongezi kwa kampuni ya Asas wazalishaji wa maziwa Bora nchini ya Asas kwa kudhamini mashindano ya mchezo wa Gofu ya Mufindi Southern Open Championship 2023 na kushudia Kajuna Maurice kutoka Lugalo gofu akiibuka bingwa wa mashindano hayo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa bingwa na washindi mbalimbali wakiwemo wanawake na wazee wenye umri wa zaidi ya  miaka 60 na kuendelea , Dr. Salekwa alisema kuwa kampuni ya Asas imekuwa faraja kwa jamii ya wanamichezo hivyo lazima waungwe mkono ili kuendelea kujitoa katika kudhamini michezo mbalimbali nchini.


Licha ya kuipongeza kampuni ya Asas alitoa wito kwa Wanawake wajitokeze kwa wingi kushiriki michezo mbalimbali hususani mchezo wa Gofu kwa kuwa katika dunia ya sasa michezo inatoa fursa ya ajira.

Alisema kuwa mchezo wa Gofu ni ajira tosha hivyo yuko tayari kujifunza mchezo huo wakati wowote na kuwaondoa hofu wanawake kwamba ni mchezo wa gharama.

Aliongeza kuwa kiwanja Bora cha gofu kiko kwenye wilaya ya Mufindi na serikali Iko tayari kuunga mkono mchezo huo kwa kuwa ni Moja ya chanzo Cha mapato kwa wilaya kwa kuwa wageni wengi wamekuja na kuingiza Hela maeneo haya.


Awali akisoma risala ya mashindano hayo kwa mgeni rasmi, Mmoja ya washiriki wa mashindano hayo , Yona Mbadime alisema kuwa mashindano yamekuwa na mafanikio makubwa  na kuweza kushirikisha wanamichezo takriban 44 ambapo Wanawake walioshiriki ni 4 kutoka kwenye vilabu vitano vya Lugalo Gofu, Kilombero , Gymkhana, Moshi na Mufindi.

Naye mwakilishi kutoka kampuni ya Asas, Mohamed Salim ambaye ni afisa masoko alisema kuwa kampuni hiyo Iko tayari kushirikiana na wanamichezo wa mchezo huo na wasisite pindi wanapohitaji msaada 


Alisema kuwa mchezo huo unazidi kuwa kivutio kwani hauchagui rika katika kucheza hivyo watu wajitokeze kushiriki na kufanya uwe na Wachezaji wengi zaidi.

Katika mashindano hayo washindi walijinyakulia zawadi mbalimbali zikiwemo tv flat screen , friji na radio na fedha taslimu.


No comments:

Post a Comment

Pages