HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 31, 2024

MAGU KINARA MASHINDANO YA UMITASHUMTA MKOA WA MWANZA, YABEBA VIKOMBE 13


Mkuu wa Wilaya ya Magu , akipokea zawadi ya kombe la mshindi wa jumla mashindano ya ya umoja wa Michezo na taaluma kwa wanafunzi wa Shule za Mshingi Tanzania (UMITAMSHUMTA) kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza zilizoshiriki mashindano hayo leo Ijumaa Mei 31,2023.

 

Halmashauri ya Wilaya ya Magu imeshika nafasi ya kwanza kimkoa katika Mashindano ya umoja wa Michezo na taaluma kwa wanafunzi wa Shule za Mshingi Tanzania (UMITASHUMTA) kwa kuchukua vikombe 13 katika fani za mpira wa kikapu wavulana na wasichana, riadha , kwaya, ngoma, mpira wa miguu wavulana, handball , usafi na nidhamu na kombe la mshindi wa jumla katika Halmashauri zote za mkoa wa mwanza zilizoshiriki mashindano hayo.

Akitangaza matokeo hayo mbele ya mkuu wa Wilaya Afisa utamaduni wa Wilaya ya Magu, Peter Mujaya amesema magu imebeba vikombe 13 katika fani ya mpira wa kikapu wavulana na wasichana nafasi ya kwanza, mpira wa mikono wavulana nafasi ya 2, na wasichana nafasi ya tatu, riadha wasichana nafasi ya 1 na wavulana nafasi ya 3, kwaya nafasi ya 1, ngoma nafasi ya 2 , muziki nafasi ya 3, mpira wa miguu nafasi ya 3, usafi na nidhamu nafasi ya 1, mpira wa wavu nafasi ya 3 pamoja na kombe la mshindi wa jumla kwa mkoa wa mwanza.

Akizungumza wakati akipokea vikombe hivyo leo Mkuu wa Wilaya ya Magu Mh. Joshua Nassari amewapongeza vijana  kufanya  vizuri  kwa katika mashindano hayo na akasisitiza kuongeza bidii na kufanya vizuri zaidi katika mashindano  ya Kitaifa.


Aidha DC Nassari ametoa rai kwa wanafunzi hao kutumia ushindi huo katika kuongeza juhudi na bidii katika taaluma na kufanya vizuri katika masomo yao ili kufikia malengo yao na kuifanya wilaya ifanye vizuri katika taaluma.

Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mohamed Ramadhani ametoa pongezi kwa wote waliofanikisha ushindi na kuwataka wafanye vizuri zaidi kwa mashindano mengine hapo mwakani.

 Vijana 26 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Magu wameteuliwa kuunda timu ya mkoa itakayoshiriki mashindano ya UMITASHUMTA taifa yatakayofanyika mwezi  Juni  Mkoani Tabora.

No comments:

Post a Comment

Pages