HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2024

Access Microfinance Bank Tanzania Limited yabadili chapa ya jina sasa kutambulika Selcom Microfinace Bank Tanzania Limited

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam


Benki ya Access Microfinance  Tanzania Limited imesema kuanzia Juni 4 mwaka huu imekuja na mabadiliko chanya ya chapa ya jina na kwamba kwa sasa itatumbulika kwa jina la Selcom Microfinace Bank  Tanzania Limited.

Aidha, baada ya kubadili jina kua Selcom Microfinance Bank Tanzania Limited  imesema itahakikisha Wajasiriamali wa kati na wa chini wanawezeshwa kiuchumi ikiwemo kukuza biashara zao kupitia mikopo, benki hiyo imetenga Sh trilion1.6 ili kuwawezesha wajasiriamali hao.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam Afisa Mtendaji Mkuu wa Selcom Microfinance Bank Tanzania Limited Julius Ruwaichi amesema ubadilishaji wa chapa ya jina unaonyesha dhamira ya kubadilika kulingana na mahitaji ya wateja wao hivyo itajielekeza kutoa huduma zilizo sahihi na fasaha za kifedha zilizojaa ubunifu mkubwa.

 "Selcom Paytech Limited, mwanahisa wetu mkubwa, anabeba jina linaloaminika katika tasnia ya huduma za kifedha na malipo kwa zaidi ya miaka 22. Selcom Paytech, ambayo ni maarufu kwa maendeleo na kutegemewa, imekuwa mstari wa mbele katika ubunifu na uvumbuzi nchini. Tunapohamia Selcom Microfinance Bank Tanzania Limited, tunaleta pamoja nasi kiwango kile kile cha ari, kutegemewa, ubunifu na uvumbuzi ambacho umekuwa ukiufurahia na kukidhi matarajio yako," amesema Ruwaichi.

Amebainisha kuwa kama sehemu ya kuimarisha muonekao wao, Benki ya Selcom Microfinance Tanzania Limited wataleta utambulisho mpya kwa muonekano wake na rangi kuu za muonekano zitabadilika kuwa nyekundu, nyeupe na nyeusi na kwamba  sura ya nje ya mwonekano wao inabadilika, huku ahadi zao dhabiti za huduma zilizoboreshwa zinazozidi matarajio yako na kukufanya wateja wawe nao daima.

Amesisitiza kuwa wa sheria zinazoongoza  mabadiliko hayo hayataathiri haki au wajibu wowote wa benki au kutoa kuathiri madai/mashauri yoyote ya kisheria na au dhidi ya wadau wao, wala kanuni, kila kitu kitakuwa kinahama kutoka Access Microfinance Bank Tanzania Limited hadi Selcom Microfinance Bank Tanzania Limited.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha Mwezi Mei, 2024 zaidi ya vijana wakiwemo wakulima 200,000 na wafanyabishara wameweza kupatiwa mikopo huku akibainisha tayari wameshafungua matawi katika mikoa  ya Iringa, Mbeya pamoja na Dar es Salaam.

Pia amesema mtaji wa benki  umefikia Sh Bilioni 8.6 na kwamba baada ya miwili ijayo wamelenga kukuza mtaji hadi kufikia Sh bilioni 20 huku akifafanua Riba ya benki hiyo ni Asilimia 2 hadi 4.8 kutokana aina ya mkopo ya mteja anaouchukua.

No comments:

Post a Comment

Pages