HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 02, 2024

IMEBAKI STORI KWA WANA SIMBA

Na Mwandishi Wetu
 
Clatous Chota Chama amekuwa kwenye rekodi ya wachezaji waliocheza klabu mbili kubwa nchini za Simba na Yanga baada ya uhamisho wake kukamilika rasmi hii leo kuelekea Jangwani.

Chama anaungana na Haruna Niyonzima, Emanuel Okwi, Benard Morrison, Juma Kaseja, Gadiel Michael, Mrisho Ngassa na nyota wengine.

Chama alikuwa anavalia jezi namba 17 ndani ya viunga vya wekundu wa msimbazi na imekuwa tamaduni Duniani kote kuwa mara nyingi mchezaji bora anahama na jezi namba yake.

Chama anaelekea Yanga na huenda tukamshuhudia Farid Mussa akimkabidhi Chama jezi namba 17. Hii si ya kwanza kwani tuliwahi kuwaona wachezaji kadhaa Duniani wakiwaachia wengine namba zao walizozizoea.

Juan Cuadrado alimuachia Ronaldo jezi namba 7 pale Juventus. Martial alimuachia jezi namba 9 Ibrahimovic pale United na Ibrahimovic akamuachia jezi namba 9 Romelu Lukaku pale United.

Tutegemee kumuona Chama kwenye jezi namba 17 huku tukimuona Farid Mussa kwenye namba mpya ya jezi.



No comments:

Post a Comment

Pages