DAKIKA 45 za kwanza za pambano raundi ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF CL 2025/26 - preliminary round), kati ya Gaborone United ya Gaborone, Botswana, zimekamilika kwa Wekundu wa Msimbazi kuongoza kwa bao 1-0.

Simba wametawala dakika 45 hizo za kwanza kwenye dimba la Obedi Itani Chilume, walikonufaishwa na bao la Elie Mpanzu Kibisawala, kunako dakika ya 16, kwa kichwa akiunganisha kimiani krosi ya nahodha Shomari Kapombe.
Licha ya zaidi ya nusu kikosi kujumuisha nyota wapya, Simba wameoneaha uhatari uliowapa uongozi huo muhimu kwa Wekundu hao wa Msimbazi, kuelekea kushinda mechi hiyo na kuweka hai matumaini ya kufuzu hatua inayofuata ya michuano hiyo.
Simba inayonolewa na kocha Fadlu Davis, anayedaiwa kujiandaa kuipa mkono wa kwaheri, iko dimbani ikiwa na nyota wapya saba, aliwemo Anthony Mligo, Allasane Kante, Rushine de Reuck, Naby Camara, Neo Maema na Suleiman Mwalimu.
September 20, 2025
Share This
About HABARI MSETO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Ut wisi enim ad minim veniam, quis nostrud exerci tation ullamcorper suscipit lobortis nisl ut aliquip ex ea commodo consequat. Duis autem vel eum iriure dolor in hendrerit in vulputate velit esse molestie consequat.




No comments:
Post a Comment