HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 20, 2013

Waziri Mukangara awashauri vijana nchini

Na  Mwanakombo Jumaa- Maelezo, Arusha

Vijana nchini  wameshauriwa  kuzitumia vizuri fedha za  mkopo wa mfuko wa maendeleo ya  vijana  ili  kuwawezesha  kukuza uchumi wao na hivyo kuondokana na umaskini.

Hatua hii pia itawawesha kukuza kipato chao na hivyo kubadilisha maisha yao hatua ambayo itasaidia   kupunguza tatizo la ajiira nchini kwa makundi ya vijana.

Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Habari , Vijana , Utamaduni na Michezo  Dkt. Fenella Mukangara  wakati wa ziara yake ya kuvitembelea vyama vya ushirika wa akiba na mikopo (Saccos) mbalimbali viliv yopata mkopo kutoka mfuko wa maendeleo ya vijana unaosimamiwa na wizara hiyo.

 Mfuko huo ambao lengo lake ni kuwasaidia vijana ama vikundi vya vijana  ili waweze kujiajiri kupoitia shughuli za uzalishaji mali  na  miradi ya kiuchumi.

 Dkt. Mukangara  amesema  mikopo inayotolewa na  wizara yake ni jitihada za serikali kuwasaidia  vijana  na wajasiliamali  ili waweze kujikwamua kiuchumi  katika maisha, hivyo  alisisitiza suala la uaminifu, nidhamu na uadilifu katika kutumia mikopo hiyo  likiwemo suala la vijana hao kurejesha  kwa wakati mikopo hiyo.

 Akiwa katika kutembelea saccos ya soko kuu waziri Dk. Mukangara alielkezwa na katibu wa ushirika huo Philipo Kullaya kuwa  ushirika huo una wanachama wapatao 597 ambapo asilimia 70  ni vijana
Alisema  ushirika huo umefanikiw akuwapatia wanachama wake wakiwemo vijana mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 847.

Aidha alimweleza waziri kuwa   saccos hiyo kwa mwaka 2009/2010 ilifanikiw akupata mkopo wa shilingi milioni tano kutoka mfuko wamaendeleo ya vijana unaosimamiwa na wizara yake  ambapo vijana wapatao 22  walinufaika na fedha hizo.

 Kufuatia  hali hiyo  Waziri Dkt. Mukangara  amefarijika kuona wajasirirmali  ni kwa jinsi gani   wamenufaika na fedha hizo na jinsi walivyoweza kurejesha  mikopo kwa wakati
 Amesema hatua hii imesaidia kuwawezesha vijana kuwatengenezea ajira za uhakika na pia kutengeneza ajira kwa vijana wengine mkoani Arusha.

Hata hivyo   wanaushirika hao walimweleza waziri huyo kuwa wanakabiliw ana changamoto kubwa ya kukosa elimu ya ujasiriamali pamoja na mitaji midogo ili kupanua wigo kwa vijana wengi kuweza kupata mikopo kutoka  mfuko huo wa maendeleo ya vijana.

Katika ziara yake pia ameziagiza taasisi za wizara yake  ikiwemo Idara ya Habari (MAELEZO) , Kampuni ya magazezi ya Serikali (TSN) na  Shirika la Utangazaji  nchini (TBC) zifanye kazi kwa kushirikiana

Waziri Mukangara amesisitiza kuwa hivi ni vyombo vya serikali na hivyo vinapaswa kutetea sera za serikali pamoja na kujibu hoja mbalimbali zinazozoikabili serikali   kwani vyombo hivi ndio mdomo wa Serikali.

Katika ziara yake amevitembelea ushirika  wa PETU SACCOS, Soko KUU SACCOS pamoja na Krokon SACCOS  ambapo alipata fursa ya kuongea na viongozi pamoja na wanachama 

No comments:

Post a Comment

Pages