HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 29, 2013

Benki ya Exim yataangaza neema kwa wahitimu wa vyuo vikuu


Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Exim, Dinesh Arora (katikati) akimfanyia usaili Faraji Mussa (kulia) mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika kitivo cha Uchumi na Takwimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati wa maonyesho ya Career Day Fair yaliyofanyika chuoni hapo mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Msaidizi Rasilimali Watu wa Benki ya Exim, Hetal Ramaiya. (Na Mpiga Picha Wetu)

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya Exim imetangaza mpango wa kutoa nafasi za ajira zaidi kwa wahitimu kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini ikiwa ni mpango wa benki hiyo wa kukuza sekta ya ajira.

Akizungumza katika maonyesho ya vyuo vikuu maarufu kama Career Day Fair yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Exim, Dinesh Arora alisema kuwa vyuo vikuu vina nafasi kubwa ya kuziba pengo la upungufu wa wafanyakazi katika sekta ya kibenki na fedha nchini.  

“Baada ya uanzishwaji wa kituo chetu cha mafunzo kinachojulikana kama Exim Academy, benki yetu sasa imeamua kuwalenga wahitimu moja kwa moja kutoka vyuoni na uzoefu hautakuwa kipingamizi kutokana na kuwa wahitimu hao watapatiwa mafunzo muhimu pindi watakapojiunga na benki yetu.

“Nimebahatika kufanya usaili kwa baadhi ya wahitimu leo na nimeona wengi wana uwezo mkubwa sana. Baada ya zoezi hili kukamilika, Tutachagua baadhi yao ili wajiunge na benki,” alisema Arora.

Awali, Meneja Mwandamizi wa Tawi la Benki ya Exim la Clock Tower, Agnes Kaganda aliwapa changamoto wahitimu hao kuwa makini katika maisha ili kufikia malengo na ndoto zao.

“Katika hii dunia hakuna kisichowezekana. Naomba mwendelee kufanya kazi yoyote itakayopatikana bila kukata tamaa na usiruhusu mtu yoyote kukuvurugia ndoto zako.
Kwa upande wake makamu wa rais wa Kamati ya Mandalizi ya maonyesho hayo, Wendo Lendo alisema kuwa maonyesho hayo yametoa fursa kwa wahitimu hao kujuana na makampuni mbalimbali makubwa.

“Maonyesho ya leo yameonyesha mafanikio kwa kuwa mfumo wa elimu wa Tanzania hausaidii katika kuwajengea uwezo wahitimu wa kuajiriwa. Zaidi ya makampuni 20 yameshiriki leo hii na ninauhakika kwa mwaka ujao maonyesho yatakuwa makubwa na yenye mafanikio zaidi,” alisema Lwendo.


No comments:

Post a Comment

Pages