HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2013

BONDIA NATHAN CLEVERLY AMCHAPA ROBIN KRASNIQI


Bondia Nathan Cleverly kushoto, akipambana kutetea ubingwa wake wa WBO dhidi ya Robin Krasniqi.

WEMBLEY, London

Bingwa huyo wa dunia wa WBO uzani wa ‘light’ ametetea mkanda wake huo kwa mara ya tano baada ya ushindi wake wa pointi dhidi ya Krasniqi, ushindi ambao ni hatua kubwa kuelekea pambano la ndoto yake dhidi ya Bernard Hopkins

BONDIA Nathan Cleverly amethibitisha uhatari wake ulingoni na kuwa mmoja wa mabondia wakubwa katika ulimwengu wa masumbwi baada ya kumshinda mpinzani wake Robin Krasniqi katika pambano lililofanyika Wembley Arena mwishoni mwa wiki.

Bingwa huyo wa dunia wa WBO uzani wa ‘light’ ametetea mkanda wake huo kwa mara ya tano baada ya ushindi wake wa pointi dhidi ya Krasniqi, ushindi ambao ni hatua kubwa kuelekea pambano la ndoto yake dhidi ya Bernard Hopkins.

Akizungumzia pambano na matokeo, Cleverly alisema: “Nadhani sasa niko tayari. Mimi bado najifunza hatua kwa hatua, lakini kujiunga na ngumi za uzito wa juu ni jambo ambalo nililokuwa nikilitaka.

“Tutaona kama nitaweza kuzalisha matokeo mazuri zaidi. Naamini naweza.”

Cleverly katika pambano hilo alipoteza raundi ya kwanza pekee, baada ya kupewa alama chache na majaji kulinganisha na mpinzani wake Krasniqi.

Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani, alifanya kazi ya ziada kuibuka na usjhindi huio wa pointi, na mara kadhaa aliwekwa majaribuni kiasi cha wengi kudhani Cleverly angerefusha rekodi yake ya kutopigwa na kufikia madpambano 26.

Kwa ushindi huo, sasa Clev, 26, anakaribia kutimiza ndoto ya kuumana na nyota machachari wa mchezo huo Hopkins, ambaye aliliangalia pambano la hasimu wake kwa njia ya televisheni akiwa nyumbani kwao Marekani.

The Sun 

No comments:

Post a Comment

Pages