HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2013

PUYOL, MASCHERANO KUWAKOSA BAYERN MUNICH KESHO


BARCELONA, Hispania 

"Puyol hatokuwa tayari kwa mchezo wa Jumanne jijini Munich na hatujui kama ataweza kuiwahi mechi ya marudiano (Mei 1). Mascherano anaendelea vizuri, lakini pia hatujui kama ataiwahi mechi ya marudiano"

NYOTA wawili wa safu ya ulinzi wa FC Barcelona, Carles Puyol na Javier Mascherano watalazimika kulikosa pambano la kesho Jumanne la nusu fainali ya amabingwa Ulaya dhidi ya Bayern Munich, Kocha Msaidizi wa Barca Jordi Roura amethibitisha.

Puyol, nahodha wa kikosi hicho, amefanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu alichoumia mwezi uliopita, huku Mascherano aakivunjika mifupa midogo katika mechi ya sare ya 2-2 dhidi ya Paris St Germain iliyopigwa Aprili 2.

"Puyol hatokuwa tayari kwa mchezo wa Jumanne jijini Munich na hatujui kama ataweza kuiwahi mechi ya marudiano (Mei 1), itategemea ni kwa namna gani atapona haraka, lakini pia itategemea na maamuzi ya daktari," alisema Roura.

"Mascherano anaendelea vizuri, lakini pia hatujui kama ataiwahi mechi ya marudiano," aliongeza Roura anayekaimu nafasi ya kocha Tito Vilanova anayemaliza muda wa mapumziko kutokana na operesheni ya kansa ya tezi.

Barca, inayofukuzia ubingwa wa tatu wa Ulkaya katika misimu mitano, ina machaguo kadhaa katika kumpata mshirika wa Gerard Pique katika ulinzi wa kati, iakiwamo beki wa pembeni Adriano, kinda wa kikosi cha vijana Marc Bartra na viungo Alex Song na Sergio Busquets.

Eric Abidal, ambaye ameanza kukitumikia kikopsi cha Barca hivi karibu akipona kutoka katika upandikizaji wa Ini, anaweza kuwa chagu jingine la Roura, ingawa anahitaji muda zaidi kabla ya kurejea katika mikikimikiki ya mabingwa Ulaya.

"Kimsingi Abidal tunapaswa kumchukulia hatua kwa hatua. Ni kawaida kwamba yeye ameonesha nia ya kucheza, kama ilivyo kwa wachezaji wenzake. Amejifua vya kutosha, amefanya mambo makubwa na yuko fiti kama wakati mwingine."

Aidha, nyota wa utikisaji nyavu wa kikosi hicho, Lionel Messi ameripotiwa kuwa yu tayari kwa mpambano wa kesho, baada ya kuwa shakani kutokana na kuumia katika mechi dhidi ya PSG.

"Messi yuko katika hali nzuri," alisema Roura. "Amerejea kazini na kikosi huku akioenesha utayari utokanao na kupona kwa haraka na naamini atafanya kila liwezekanalo kuwa fiti zaidi."

SuperSport.com

No comments:

Post a Comment

Pages