HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 22, 2013

TOTTENHAM WATAKA PAUNI MILIONI 100 KUMUUZA BALE


LONDON, England

Gazeti la The Sun lilifichua mpango wa bosi mpya anayekaribia kushika hatamu klabuni Allianz Arena yaliko makazi ya Bayern, Pep Guardiola wa kuchuana na Madrid na PSG katika vita ya kupata saini yam kali huyo

MWENYEKITI wa klabu ya Tottenham Hotspur ya jijini hapa, Daniel Levy, ametaja dau la pauni milioni 100 ndilo linaloweza kumng’oa winga wake hatari Gareth Bale, klabuni White Hart Lane.

Levy amelitaja dau hilo rekodi ya dunia kupata saini ya winga huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 27, akimini ni sahihi kwa mkali wake huyo kutua popote miongoni mwa klabu zinazomuwinda.

Anaamini nyota huyo anayewindwa na klabu kongwe na tajiri duniani za Bayern Munich ya Ujerumani, Real Madrid ya Hispania na Paris Saint-Germain ya Ufaransa, ana kiwango kikali kitakachoongezeka zaidi, pindi atakapotua katika klabu hizo.

Gazeti la The Sun lilifichua mpango wa bosi mpya anayekaribia kushika hatamu klabuni Allianz Arena yaliko makazi ya Bayern, Pep Guardiola wa kuchuana na Madrid na PSG katika vita ya kupata saini yam kali huyo.

Lakini Levy anataka kubaki na nyota huyo kusaidia harakati za klabu yake, angalau kwa mwaka mmoja zaidi.

Kushindwa kushika nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya hapa kunakoweza kuipa tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya, kunaweza kumsukuma Bale kutimka klabuni hapo kiangazi hiki.

The Sun

No comments:

Post a Comment

Pages