HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 24, 2013

ABDUKIBA AJA NA 'SIAMINI'


Na Elizabeth John

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdukarim Kiba ‘Abdukiba’ yuko mbioni kuachia kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Siamini’ hivi karibuni.

Akizungumzia kibao hicho, Abdukiba alisema, yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa wimbo huo na ataisambaza katika vituo mbalimbali vya radio mwishoni mwa wiki hii.

Alisema katika wimbo huo, kuna baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya watasikika, ambao hajapenda kuwataja ili kuwapa mtihani mashabiki wake kujiuliza nani ambaye kamshirikisha.

“Sipendi kusema nimemshirikisha nani katika wimbo huo, ila ningependa mashabiki wangu wakae mkao wa kula kwa ajili ya wimbo huo, najua wengi wataupenda kulingana na jinsi ulivyo tofauti na nyimbo nyingine,” alisema Abdukiba.


Mbali na ‘Siamini’, Abdukiba alishawahi tamba na vibao kama ‘Kizunguzungu’, ‘Huyo si demu’ ‘Kidela’ na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya.

No comments:

Post a Comment

Pages