HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 24, 2013

MATONYA 'ANAJIAMINI'



Na Elizabeth John

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Seif Shabani ‘Matonya’ amesema yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Najiamini’.

Matonya kwa sasa anatamba na kibao ‘Zilipendwa’ ambacho kinafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio na televisheni kutokana na maudhui yaliyopp ndani yake.

Aliwaomba mashabiki wake wakae mkao wa kula kwa ajili ya kukipokea kibao hicho ambacho anaamini kitafanya vizuri.

“Mashabiki wangu wananijua kwamba nipo kamili na huwa sitoi vitu ambavyo havijakamilika, naomba wakae mkao wa kula kwa ajili ya kuipokea kazi hiyo ambayo itakuja pamoja na video yake,” alisema.

Mbali na kazi hizo, mkali huyo alishawahi kutamba na vibao vyake kama, ‘Taxi Bubu’, ‘Violeth’ na vinginezo ambavyo vilimtambulisha katika tasnia ya muziki wa bongo fleva.

No comments:

Post a Comment

Pages