HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 02, 2013

MAKAMU WA RAIS DK. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA JOPO LA WATAFITI WA MASUALA YA UCHUMI AFRIKA, JIJINI ARUSHA LEO

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua rasmi Mkutano wa Jopo la Watafiti wa Masuala ya Uchumi Afrika (AERC) kujadili athari za Mazingira kwa Maendeleo ya Bara la Afrika, uliofanyika Jijini Arusha leo Juni 02, 2013. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mtafiti wa Kisayansi Kutoka Mpango wa Pamoja unaohusu Sera za Kisayansi na Mabadiliko ya Tabianchi, Keneth Strzepek (kulia) na Mtafiti Mwandamizi wa Kisayansi,Adam Schlosser (katikati) baada ya kufungua rasmi Mkutano wa Jopo la Watafiti wa Masuala ya Uchumi Afrika (AERC) kujadili athari za Mazingira kwa Maendeleo ya Bara la Afrika, uliofanyika Jijini Arusha leo Juni 02, 2013. Picha na OMR
 Profesa, Lemma Senbet, akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA) Terezya Huvisa, kumkaribisha Makamu wa Rais kufungua mkutano huo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA) Terezya Huvisa, akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Makamu wa Rais kufungua mkutano huo.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo waliohudhuria wakimsikiliza Makamu wa Rais.


No comments:

Post a Comment

Pages