Meneja Mkuu wa SimbaNET, Stanley Ayittah akikata utepe wakati wa ufunguzi wa darasa la kompyuta katika Shule ya Msingi, Heritage iliyopo Banana, Ukonga. Katikati ni Mkuu wa shule hiyo, Apiemi Elijah Kebaso na Mkurugenzi wa shule hiyo, Josephat Mnanka. (Picha na Francis Dande)
Mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi, Heritage, Rose Joab akiwaonesha kwa vitendo somo la sayansi, wazazi na wageni waliofika katika mahafali ya sita ya shule hiyo.
Baadhi ya wanafunzi waliohitimu mahafali ya darasa la saba wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi.
Meneja Mkuu wa SimbaNET, Stanley Ayittah ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo akizungumza na waandishi wa habari.
Mkuu wa shule ya Heritage, Apiemi Elijah Kebaso akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi, Heritage wakiingia kwa kwaride maalum wakati wa mahafali ya sita ya shule yao.
Macho mbeleeee......
Na Mwandishi Wetu
MWALIMU Mkuu wa Shule ya
Msingi Heritage iliyoko Ukonga Banana wilayani Ilala jijini Dar es Salaam, Apiemi
Kabaso amewataka wanafunzi kujikita katika masomo ya sayansi ili nchi iweze
kupata wahandisi wa sekta hiyo.
Kibaso aliyasema hayo wakati
wa mahafali ya sita ya shule hiyo ambapo wanafunzi 53 walihitimu elimu ya
msingi, mahafali hayo yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Alisema vijana hao wakati
wakimaliza ahatua ya kwanza, watambue kuwa taifa lina kabiriwa kwa kiasi
kikubwa na ukosefu wa wataalamu wa sayansi, hivyo wanalo jukumu la kulinasua
taifa kwa kusoma kwa bidii masomo hayo.
Aidha, kwa kulitambua hilo,
ndio maana shule hiyo imeamua kuwekeza zaidi kwenye masomo hayo ya sayansi
ambapo kwa sasa wamefungua ntanet ambayo itawasaidia wanafunzi katika masomo
yao.
“Tunaishukuru kampuni ya
SimbaNet kwa msaada wao wa kuwfungulia Intenet, kwani wanaamini itawasaidia
katika kumiza ndoto za wanafunzi katika kujitafutia taarifa mbalimbali za
masomo”alisema.
Aliongeza kuwa watakuwa
waangalifu katika matumizi ya internet hiyo ili kudhibiti matumizi yasio sahihi
kwa wanafunzi.
Naye Meneja Mkuu wa Kampuni
ya SimbaNet Stanley Ayittah, alisema kampuni yake ilitoa kompyuta hizo kutokana
na mfumo wa sasa kutawaliwa zaidi na sayansi na teknolojia.
Aidha, alivutiwa na
mazingira ya shule hiyo kwani ni rafiki
na yanamfanya wanafunzi apende kujisomea ambapo pia aliwataka wanafunzi hao kuepukana
anasa na vishawishi vya dunia ili wafike mbali kielimu.
No comments:
Post a Comment