Na Mwandishi Wetu, Kisarawe
WAKAZI wa Mlongazila wilayani Kisarawe mkoani Pwani wamelitaka jeshi la polisi kumkamata Moshi Hamad, kwa madai ya kumng’ata mwanaye wa kumzaa Khadija Twaha (6), sehemu za siri, akidai amekuwa akijisaidia haja kubwa na ndogo hovyo.
WAKAZI wa Mlongazila wilayani Kisarawe mkoani Pwani wamelitaka jeshi la polisi kumkamata Moshi Hamad, kwa madai ya kumng’ata mwanaye wa kumzaa Khadija Twaha (6), sehemu za siri, akidai amekuwa akijisaidia haja kubwa na ndogo hovyo.
Wakizungumza kwa nyakati
tofauti wilayani hapa juzi, wakazi hao, walisema mama huyo amekuwa
na tabia ya kumfungia ndani mtoto wake huku akimchapa zaidi ya nusu saa jambo
lililosababisha watoe taarifa kwenye dawati la haki za binadamu.
Walisema walifikia uamuzi
huo baada ya kuchoshwa na vitendo hivyo ikiwemo kumpiga mwanaye huyo kwa
kutumia nyaya za simu huku akimng’ata sehemu mbalimbali za mwili wa mtoto huyo
na kumsababishia maumivu makali.
Stella Musa alisema sehemu
za siri za mtoto huyo zimeharibiwa kutokana na kung’atwa na meno huku sehemu zake
za makalio zikiwa na vidonda ambavyo vinadaiwa vimetokana na kuchomwa
na ncha kali.
“Wazazi wa mtoto huyu ni
wanangu, siku moja mama wa huyu mtoto alishawahi kumuumiza mkono nilimchukua na
kukaa naye nyumbani kwangu kwa mwezi mmoja nikimuhudumia kwa kumkanda kwa maji
ya moto,”alisema Stela.
Mwalimu wa Shule ya Msingi
Mlongazila ambaye ni katibu wa dawati la kutetea haki za binadamu Paulo Idana
alisema suala hilo limewafikia hivyo wanachukua hatua za kisheria huku mtoto
huyo akiwa chini yao kwa ajili ya matibabu zaidi.
“Tulimfuata mama huyu
Septemba 20 mwaka huu na kutulifanya mahojiano mbele ya ofisa Mtendaji wa
kijiji hiki na alikiri akisema alifanya hivyo kwa sababu ya hasira lakini, sisi msimamo wetu tunafanya
utaratibu ili tuweze kumfikisha kwenye vyombo vya sheria,”alisema Idana.
Mtoto huyo, jina
linahifadhiwa ambaye anasoma katika shule ya wali Mtenga (chekechea), alisema wakati
mwingine mama yake alikuwa akimwiita ili amfundishe kusoma na aliposhindwa aling’atwa
mgongoni, mapajani na sehemu za siri huku akisema atafanyia hivyo hadi ajue
kusoma ndipo ataacha kumwadhibu.
“Hivi vidonda vya
kwenye mwili wangu ni vya kung’atwa wakati mwingine napigwa na waya, hiki
kidole mama alinikata kutokana tu nilishindwa kusoma, alisema huku akilia kwa
maumivu makali sana mtoto huyo.
Mama wa mtoto huyo, Moshi
Hamad, alisema alikuwa akitoa adhabu hiyo kwa mwanaye huyo kutokana kujisaidia haja ndogo na kubwa
hovyo wakati arudiopo kutoka shule.
“Nafanya hivi kutokana na
hasira siwezi nikamuona mtoto wangu anajisaidia haja kubwa na ndogo kwenye nguo
nikamwacha tu lazima nimwadhibu mbona, kama jana alitapika kwenye sahani je
mtoto kama huyu nitamwacha,”alihoji Moshi.
Mwenyekiti wa Kitongoji hicho
Hadija Samizi alikiri kuwepo suala hilo hivyo serikali ya mtaa huo inafanya
utaratibu ili kuhakikisha anafikishwa kwenye vyombo sheria.
No comments:
Post a Comment