HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 05, 2013

Nilisema; Madudu ya Pindi Chana hayawezi kuvumilika hata na JK
Na Bryceson Mathias

UMATANO 11, Septemba 2013 nilisema katika Makala yangu juu ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria, Pindi Chana, kwamba kutokana na kinachoonekana kuwa mwavuli wake wa kukifunika Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukivusha katika mchakato wa mapendekezo ya Katiba Mpya! Si tu umetoboka! Bali Umechanika.

Haikuwa tu Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) kupitia kwa Mwenyekiti wao, Said Miraji, kumshushua  Chana na kuutoboa Mwavuli huo au Chama cha Wananchi (CUF), bali hata mimi, kwa kauli yake haikuwa sahihi nilimmtaka atuombe radhi watanzania, lakini alijibaraguza  na kukaa kimyaa!

Hivi ni lini viongozi wetu watafikia kuwa na uadilifu ili wanapofanya madudu kama aliyofanya Chana! Alipotutumainisha na kujigamba mle mjengoni kuwa wazanzibari wameshirikishwa kuhusu Mchakato wa Mapendekezo ya Katiba Mpya, kumbe sivyo?

Ingawa kwa kauli za Viongozi wa Juu wa Serikali zote mbili inaonesha wazanzibari walishirikishwa. Wazanzibari wenyewe wakiwemo ADC na CUF walikataa katu katu, na kudai kitendo kilichofanywa hakina udugu wala kuaminiana isipokuwa kudharaulina.

Watanzania sasa wanayo kila sababu kumhoji Chana, nini dhamira yake kusema walishirikishwa wakati hawakushirikishwaa? Wananchi wana fursa kutilia shaka nia za baadhi ya Viongozi hadi kufikia kubadilisha yale yaliyokubaliwa kwa pamoja na Vyama vya Upinzani wakiwepo.

Katika hilo Watakuwa wana haki ya kuuliza nia ni hii yetu sote ya kupata katiba mpya kwa kutumia njia za kikatiba na kisheria au wana dhamira nyingine iliyojifisha nyuma ya kuweka kile ambacho hakikukubalika kwenye maridhiano ya pamoja?”

Nafarijika na Kauli ya Rais Jakaya Kikwete aliyosema bila kumung’unya maneno “Hivyo basi napata tabu kuyaelewa madai kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haikushirikishwa msingi wake nini!  Labda kuna kitu sikuambiwa,” alisema.

Alisema aliulizia kuhusu hoja ya kamati kutokufanya vikao Zanzibar kusikiliza maoni ya wadau, akaambiwa kuwa kanuni za Bunge hazina sharti hilo, hivyo kamati haistahili kulaumiwa.

“Kama hivyo, nashauri kuwa suala hili lirudishwe bungeni ili wabunge walizungumze na kulifanyia uamuzi muafaka. Vinginevyo watu wataendelea kulaumiana isivyostahili,” alisema.

Mimi huwa inanipa tabu pale ninapoona mtu wa kutegemewa na elimu kubwa, ambaye wananchi katika eneo alipo wangetaka awaongoze kwa kushindanishwa na wengine, halafu anafanya kitu cha kuwashangaza na kuwasikitisha watu.

Kule kwetu Njombe ikitokea mtu huyo kafanya jambo ambalo watu wamelipinga hadi likafika kwa Kiongozi wa ukoo alikapinga katika maamuzi yake, mtu huyo huwa hawezi hata kufika msibani, kwenye sherehe  au kwenye mkusanyiko wa kijamii kwa sababu kwa aibu hunekana msaliti.

Sasa Mkuu wa Kaya kaurudisha Mjadala wa mapendekezo ya Katiba mpya bungeni ukajadiliwe kutokana na kuona mapungufu aliyoyaainisha. Je wenzangu na mimi mlioushupalia kama mnatengeneza Katiba ya Vyama vyenu mna nguvu? Mimi huwa nampongeza sana Mstaafu Rais, Ally Hassan Mwinyi, na Dume la Mbegu ya Maamuzi Magumu, Edward Lowasa!

Hali ingefika kama hapo ilipofikia pa kuonekana kulikuwa na kukosekana kwa kauli za usahihi kama alivyofanya Chana, wangefanya maamuzi magumu! Lakini siku hizi watu hao hatuna serikalini na bungeni, isipokuwa wapo wanaowalazimisha ng’ombe wapure maji wao aaa!!
Hatutafika, tunataka nao wawe na uadilifu wa uwajibikaji wanapofanya madudu ya wazi kama uposhwaji wa mapendekezo ya katibaa mpya ulivyokuwa bungeni.

No comments:

Post a Comment

Pages