HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 30, 2013

Mungai awakumbuka yatima wa kituo cha Tosamaganga kwa chakula cha mwaka mpya
Watoto  yatima  wa  kituo cha Tosamaganga jimbo la Kalenga wilaya ya Iringa  wakimpongeza Mkurugenzi  mtendaji  wa  kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa ya GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai  kulia kwa kuwajali kwa  msaada wa chakula chenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 1.5 kwa ajili ya mwaka  mpya. (Picha na Francis Godwin)

Na Francis Godwin,Iringa 

Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Kampuni  ya ujenzi  wa barabara mkoani  Iringa ya  GNSM Contractrors Co. Ltd Bw  Geofrey Mungai   amekabidhi  msaada  wa chakula  cha mwaka  mpya chenye thamani  ya  zaidi ya Tsh milioni 1.5 kwa  kituo cha kulelea  watoto yatima  cha  Tosamaganga katika   jimbo la kalenga wilaya ya  Iringa vijijini .

Akikabidhi  msaada  huo  leo  Mungai  alisema  kuwa  amelazimika  kufika katika  kituo  hicho  ambacho  kinasimamiwa na masisita  wa kanisa la RC  kama  sehemu ya  mwendelezo wa kampuni  yake kuendelea  kuzungukia  vituo mbali mbali vya kulea yatima  na  kuwapa faraja  hasa katika msimu huu wa sikikuu.

Alisema  kuwa miongoni mwa vituo ambavyo amepata  kuvikumbuka katika msimu  huu wa sikukuu ya Krismas na Mwaka mpya ni pamoja na  kituo cha Daily Bread Life (DBL) kilichopo jimbo la Iringa mjini na kituo hicho cha Tosamaganga  kilichopo jimbo la Kalenga huku lengo likiwa ni  kuwakumbuka  yatima  hao  na  kuihamasisha  jamii  kuelekeza nguvu  zao kwa  yatima kama  hao.

Bw  Mungai alisema  kuwa   takwimu  za maambukizi ya VVU katika  mkoa  wa Iringa zimeendelea  kuongezeka na iwapo  jamii haitajenga  utamaduni  wa kujali  yatima  vifo vya watoto  yatima ambao watakosa chakula baada ya kupoteza wazazi  wao kwa VVU pia  vitazidi  kuongezeka   hivyo lazima  misingi  ya  kuwajali  yatima ikaanzwa kuwekwa mapema  zaidi.

" Hawa  watoto  iwapo  jitihada za vituo vya  kusaidia yatima visinge kuwa na moyo huo  leo yawezekana  baadhi yao  wasingekuwepo hapo  tungekuwa  tumewazika  ila kazi nzuri  ya  kujitolea  inayofanywa na vituo  vya yatima  ndio  imewafikisha hapa leo ....hivyo lazima  sisi kama  jamii  kuunganisha  nguvu zetu na vituo vya yatima"

Pia  alisema  kuwa  hata  viongozi  wa vyama vya siasa na serikali ni vema wakaweka utaratibu  wa  kufanya ziara  za mara kwa mara katika  vituo  vya yatima na  kujifunza mazingira ambayo  watoto hao  wanaishi ikiwa ni  pamoja na  kusaidia  kutatua changamoto  zinazovikabili vituo vya yatima mkoani Iringa .

Kwani  alisema kwa upande wake kama  mkandarasi ambae amekuwa akifanya kazi ya ujenzi wa barabara  mkoani Iringa na nje ya mkoa ameona  ni vema  katika fedha  kiasi ambazo anazipata  kuweka utaratibu wa kusaidia watoto yatima kama njia ya  kuwahamasisha pia wenzake  kujitoa kwa yatima  katika maeneo yao ama  kusaidia kuchangia maendeleo ya maeneo yao.

Katika  hatua  nyingine Mungai aliwapongeza  walezi  wa  vituo vya  yatima katika mkoa  wa Iringa kuwa kutokana na mchango wao  wa kulea yatima hata  idadi ya yatima  na  watoto wa mitaani katika mji wa Iringa imeonekana  kupungua zaidi 

Kwa  upande  wake  diwani  wa viti  maalum tarafa  ya Kalenga Shakra  Kiwanga  akimpongeza  Mungai  alisema  kuwa ameonyesha upendo mkubwa kwa  yatima  hao na kuwataka makandarasi  wengine  kuiga mfano  huo.

Kiwanga  ambae pia ni mmoja kati ya makandarasi wadogo mkoani Iringa alisema  kuwa alichofanya Mungai ni somo kwao pia katika kutoa sehemu ya makusanyo wanayoyapata  kupitia kazi mbali mbali.


Awali mlezi  wa  kituo  hicho Herena Kihwele  alisema kuwa kituo hicho kina  watoto zaidi ya 100 na  kuwa kwa  sasa kituo kinakabiliwa na changamoto kubwa ya kushindwa  kuwalipia ada  sekondari   watoto zaidi ya 10  waliofaulu darasa la  saba ila kituo hakina uwezo wa  kuwasomesha .

Iwapo umeguswa kuchangia  kituo hicho ada ama msaada  wowote  ule waweza  kuwasiliana na mlezi wa kituo hicho Sisita Herena Kihwele kwa simu  0768831477 pia  waweza  kutumia namba hiyo kwa kutuma M-PESA.

No comments:

Post a Comment

Pages