HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 17, 2014

MGOMBEA URAIS TUCTA ATANGAZA VIPAUMBELE VYAKE



Mgombea wa Urais TUCTA, Dismas Lyassa akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kushoto ni Meneja Kampeni, Khamis Tembo na Wakili Jebra Kambole.  

Vipaumbele

Nina malengo ya kuifufua na kuleta TUCTA yenye uhai na mabadiliko ya kweli kwa kufanya yafuatayo;


 1. Kupigania na kulinda haki za wafanyakazi;

Katika kipaumbele hili lengo hasa ni kuondoa matatizo sugu ya wafanyakazi yakiwamo-:


i.             Kulipwa ujira/mishahara duni isiyoendana na uhalisia wa maisha.

ii.           Ucheleweshaji wa upatikanaji wa ujira/mishahara.

iii.          Ucheleweshaji fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya/ kiwango kidogo cha fedha za kujikimu.

iv.          Uhaba au kutokuwepo kabisa makazi kwa wafanyakazi wapya

v.            Rushwa na kuajiri kwa misingi ya kujuana kwa mfano katika Halmashauri ya Siha, wilaya ambayo imegawanywa kutoka Hai, kuna pori kubwa la West Kilimanjaro mlimani kabisa, hakuna maendeleo…ni suala la kawaida kuona watu wakiongea kilugha ofisini kama lugha ya Taifa.

vi.          Wakubwa yaani mabosi kujifanya Mungu kwa kuwaendesha wafanyakazi kwa kadri wanavyotaka wao, sivyo inavyosema sheria.

vii.         Uwepo wa mpangilio usio sawa wa ujira/mishahara.
viii.       Kutopewa posho au kupewa kidogo au kutopewa kwa wakati.

ix.          Fedha za uhamisho na likizo; kwa mfano kuna walimu ambao wameanza kazi 2004 NIT Shule ya msingi Dar es Salaam wamelipwa fedha za likizo mara moja mwaka 2012, mfano halisi ni mwalimu Ruth Natumwa, huyo ni kati ya walimu hao.

 Matatizo ya walimu kimsingi ni janga la taifa, yapo Taifa zima, kwa mfano katika shule ya Sekondari Kizota, Dodoma kuna walimu wengi  wana madai yao dhidi ya Serikali, waliajiriwa mwaka jana Machi, wakaanza kupata mshahara mwenzi wa tisa…walilipwa mshahara wa mwezi wa tisa tu na kuendelea,  ile mingine wanaendelea kudai.

x.            Mazingira magumu ya kazi mijini na vijijini (tunapozungumzia mazingira magumu inahusisha kutokuwepo vitendea kazi au kuwa vichache, miundo mbinu duni nk).

xi.          Waajiri kutochangia mifuko ya jamii
xii.        Fedha za makato ya wafanyakazi kupitia mifuko ya jamii zimekuwa zikikopeshwa watu wengine wasio wanachama wakiwamo wanasiasa huku wafanyakazi wenyewe wakiendelea kuwa na maisha duni.

xiii.       Kufanya kazi kama kibarua kwa miaka mingi jambo ambalo ni tofauti za sheria za kazi.

xiv.       Huduma za kifedha kuwa mbali na maeneo ya kazi, hali inayosababisha wafanyakazi kutumia fedha nyingi kufuatilia mishahara kwa vile ni mbali na eneo wanalofanyia kazi.

xv.         Kutokuwa na mfumo unaoeleweka wa upandishaji vyeo na ujira/malipo kwa wafanyakazi/vibarua.

xvi.       Waajiri hasa binafsi kufukuza wafanyakazi hovyo/no job security…kufanya kazi bila mikataba
xvii.      Kupambana na tatizo la kodi kubwa kwa mishahara (PAYE).

xviii.    Tatizo la mabosi kutoa upendeleo wa wazi kwa baadhi ya wafanyazi kwa sababu zisizo za kitaalamu; wakati mwingine ni kwa sababu ya ngono; kuwataka kimapenzi wafanyakazi ili waendelee kuwepo kazini au kupandishwa vyeo, tatizo hili linaonekana kuwa sugu, wanawake wengi maofisini hawako huru sana, wamekuwa wakitakwa kimapenzi mno na mabosi wao, wengi wanashindwa kujizuia, tunataka kuona kunakuwa na sheria kali dhidi ya mabosi wa aina hii kama ilivyo katika nchi nyingine.

Tatizo la ajira kuporwa na wageni

Ingawa sheria/sera za ajira zinaeleza wazi kwamba hairuhusiwi wageni kuingia nchini zaidi ya watano kwa kazi ziziso na ujuzi, baadhi ya makampuni yamekuwa yakiingiza wageni kwa kazi ambazo Watanzania wengi wanaweza kuzifanya.

Nitahakikisha wazawa wanapewa fursa ya kufanya kazi nchini; hii ni pamoja na kuomba CV za wageni.
Ili tuone kama ni kweli hakuna Watanzania wenye sifa za kufanya hiyo kazi hiyo.

        -: Kumekuwa na taarifa za uwepo wageni katika makampuni kadhaa yakiwamo mahoteli, migodi, viwanda vya sarufi nk ambao baadhi wanalipwa malipo makubwa tofauti na wazawa japo hawana elimu au ujuzi wa kuwazidi wazawa. Nitakuwa na kamati maalumu ya kufuatilia waajiriwa wote Tanzania hasa wageni ili kujua kama wanazo sifa za kufanya kazi au wanapora nafasi za Watanzania.

Nitapigania kuhakikisha tabia ya waajiri kulazimisha waajiriwa lazima wawe na uzoefu mkubwa inapungua au kukoma kabisa

Kigezo cha kupata ajira kiwe ni uwezo wa mtu wakati huo baada ya kufanyiwa usaili, siyo lazima awe na uzoefu  wa miaka mitatu au mitano kama ambavyo waajiri wengi wanalazimisha; tunahitaji kuona Serikali inasimamia hili. Kama hali ni hii, wahitimu wanawezaje kupata ajira? Ni suala ambalo nitakuwa mkali nalo mno kwa sababu lina athari kubwa kwa jamii ya Tanzania, limekuwa ni sababu ya rushwa ikiwamo ya ngono…walioko vyuoni wengi hawana uhakika wa ajira, kwa sababu ya tabia hii. Ni lazima tubadilike, watu waajiriwe kulingana na uwezo wao wa kazi, siyo uzoefu.

Wanafunzi shule ya Msingi/Sekondari nk wapatiwe elimu ya kujiajiri.

Kwa nafasi nitakayokuwanayo nitaishawishi Serikali iingize elimu ya ufundi/utengenezaji bidhaa na ujasiriamali kama mojawapo ya masomo ya ziada kama njia ya kupambana na tatizo la ajira ambalo linaonekana kukua nchini. Kama ambavyo kumekuwa na masomo ya dini katika shule zenu, tuwe pia na masomo ya ujasiriamali. Nitaangalia namna ya kuzishawishi taasisi zingine za ndani na nje kuhakikisha hili linafanyika; lengo ni kuhakikisha hata mhitimu wa msingi au sekondari nk awe ana uwezo wa kufanya ujuzi anaotaka kama kujenga, kushona, kufuma, kufuga, kutengeneza batiki, vikoi, sabuni, mishumaa nk.

Nitaanzisha idara mbili mpya na kuboresha zilizoko;

i. Idara ya walemavu

Hii itahusika kuangalia hali ya maisha ya wafanyakazi walemavu nchini ikiwamo kuwasaidia kupata baiskeli na huduma zingine muhimu.Nitatumia uzoefu wangu kwa kushirikiana na rafiki zangu wa nje kuhakikisha hili linafanikiwa.

 Tutaangalia namna ya kushirikiana na mashirika mbalimbali yakiwamo Free Wheelchair Foundation www.wheelchairfoundation.org.

Idara ya pili ni
Idara ya fursa/Career Development Department na Mafunzo
Nimetembea katika nchi tofauti Duniani ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Mauritius, India, Thailand, Sweden na Marekani.

Nimeona fursa kadhaa ambazo zimenishawishi kuanzisha idara maalum ya kusaidia wafanyakazi kufahamu fursa zinazoendelea Duniani na hapa nchini.

Fursa hizo zitakuwa zinapatikana katika tovuti za TUCTA na ofisi za vyama vya wafanyakazi mikoani.

Baadhi ya fursa ni namna gani mtu anaweza kusoma nje ya nchi bila kulipa ada kwa kozi za muda mrefu na mfupi, fursa ya mashirika ambayo yanatoa misaada kwenye sekta mbalimbali.

-Kwa mfano kuna mashirika kama www.nuffic.nl au vyuo ambavyo mtu anaweza kusoma bure bila kulipa chembe ya ada kama www.berea.edu  ya Marekani na fursa nyingine nyingi. 

Nimegundua Watanzania wengi hawanufaiki sana na fursa hizi. Ziko pia taasisi nyingine zinatoa.

Napenda kuchukua fursa hii kutoa onyo kwa wanaopanga kutoa rushwa kwenye huu uchaguzi wa TUCTA kuwa tuko makini na hili tumejipanga, tutachukua hatua za haraka za kisheria dhidi yao, ikiwa ni pamoja na kuwaripoti kwenye vyombo husika, Rushwa si kipaumbele utapinga kwa nguvu zetu zote.

Ndugu Dismas Lyasa pia atasaidia kuanzisha kituo au kushirikiana na mashirika mengine kutoa masaada wa kisheria kwa wafanyakazi wanaofukuzwa makazini kinyume cha sheria. 

Wafanyakazi wengi wakikumbwa na matatizo wafanyakazi wenzao wanawatenga, vyama vyao vinawatenga, Dismas atahakikisha kuwa TUCTA ni kimbilio lao.

Ndugu Dismas Lyasa atasaidia kutoa mafunzo ya kisheria kwa wafanyakazi ili waweze kutambua haki zao za msingi, kwa kuendesha semina, makongamano na mijadara itakayotoa elimu na kuibua mijadara kwa wafanyakazi.

CHAGUA DISMAS LYASA KWA TUCTA MPYA, Mabadiliko ni sasa, Asanteni.

No comments:

Post a Comment

Pages