HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 16, 2014

JEFFRYDER: MASHABIKI IPOKEENI 'MSALITI'

NA SYLVESTER DAVID
MSANII chipukizi wa muziki wa Hip Hop nchini,Jafari  ahmed, ‘Jefryder’,amesema vyombo vya habari havisaidii kukuza muziki wa wasanii wachanga na huendelea kukuza migogoro baina ya wasanii nchini.

Aliyasema haya jana Jijini Dar es salaam  alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi,kuwa vyombo vingi vya habari nchini hucheza nyimbo za wasanii maarufu bila kusahau kuwa hata wao walitokea mbali ukilinganisha na wasanii wachanga.

“Kuna wakati ukiwa unasikiliza redio au kusoma magazeti mbalimbali, huzungumzia habari na kupigwa nyimbo za wasanii maarufu tu wakati pia kuna  wasanii wachanga,hali hii huchangia kutokukua kwa muziki wa chipukizi,”Alisema


Jefryder ambaye ni mjasiriamali na msanii anayetamba na wimbo wa ‘Nipe Love’ aliomshirikisha msanii Steve Rnb na Darasa, aliongeza kuwa vyombo vya habari pia hutumika kuchochea migogoro miongoni mwa wasanii nchini na kufanya muziki kutofika anga za kimataifa ukilinganisha na nchi jirani za Kenya na Uganda.
Pia aliwataka mashabiki wake wawe tayari kuupokea wimbo wake mpya unaoitwa, ‘Msaliti’, alimshirikisha mwanadada Mganda Em lee na wimbo mwingine aliomshirikisha msanii maarufu nchini,  ‘Ommy Dimpoz’.     

No comments:

Post a Comment

Pages