HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 18, 2014

KATA YA MPUGUSO HAIJAWAHI KUWA NA ZAHANATI TANGU TANZANIA IPATE UHURU

Na Ibrahim Yassin, Rungwe

IMEELEZWA kuwa wananchi wa kata ya Mpuguso iliyopo wilayani Rungwe mkoani Mbeya wamekuwa wakitembea umbali  wa kilometa kumi na tano kufuata huduma ya afya kutokana na kata hiyo kutokuwa na kituo cha afya wala zahanati tangu nchi ya Tanzania ipate uhuru 1961.

Kauli hiyo ilitolewa na diwani wa kata ya Mpuguso wilayani humo,Tibandelage Kalinga kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani am,bapo aliiomba Halmashauri ya wilaya hiyo kuwa ni lini itajenga kituo cha afya na zahanati katika kata yake.

Tibandelage ambaye ni diwani wa kata hiyo kupitia Chadema alilieleza baraza hilo kuwa wananchi wake wamekuwa wakipata na kadhia hiyo ambapo akina mama wajawazito na watoto baadhi yao wamekuwa wakipoteza maisha kabla hata hawajafika hospitalini kutokana na umbali mrefu.

Alisema katika kata hiyo kuna viwanja vya wazi vingi na kutoa yeye kutoa maombi kwenye halmashauri hiyo kuhitaji kujengewa zahanati na kituo cha afya lakini amekuwa akiwekewa ngumu kutokana na kata hiyo kuongozwa na kambi ya upinzani katika ngazi ya kijiji hadi kata.

Alisema kutosikilizwa kwa tatizo hilo hasa mateso wanayopata wananchi wa kata hiyo ya kutembea umbali mrefu kumetokana na itikadi za kisiasa kwa kuwa kata hiyo inaongozwa na kambi ya upinzani na kwamba wanakwamisha jitihada hizo ili wananchi waone kama wao hawafanyi kazi.

Akijibu hoja hizo mkuu wa wilaya hiyo Chrispin Meela alisema kata hiyo ilikuwa na uwanja ambao ulitakiwa ujengwe zahanati lakini ilishindikana kutokana na kuwa uwanja huo unamatatizo kati ya mtu na kijiji hadi kufikia hatua ya kupelekana mahakamani na kukwamisha jitihada hizo.

Alisema suala la ujenzi wa miradi linaanzishwa na wananchi wenyewe kazi ya serikali ni kuunga mkono nguvu kazi hizo kwa kusaidia kupaua na si kuanzisha kujenga na kuwa wananchi na viongozi wa kata hiyo wanatakiwa kutafuta uwanja mungine na kuanzisha ujenzi kisha serikali itasaidia kupaua.

No comments:

Post a Comment

Pages