HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 11, 2014

MH.NAGU ATEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA UNGA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Mhe. DK. Mary Nagu ametembelea Kiwanda cha kutengeneza unga cha Basic Element ltd jana Novemba 10, 2014 Dar es Salaam. Waziri Nagu alitembelea sehemu za kiwanda hicho ili kuona teknolojia wanayotumia kiwandani hapo, nafaka zilizopo na namna wanavyoweka unga tayari kuuza. Katika zoezi hilo aliwapongeza na kuwataka Watanzania kutumia fursa hiyo kwa kununua unga unaotengenezwa na kuwahakikishia wakulima kutasaidia kupata soko la kuuza mazao yao.

Mhe. Nangu alitoa wito kwa watanzania kuunga mkono kazi zinazofanyika nchini kwa kununua unga unaopatikana ikiwa ni salama na wenye ubora unaofaa kwa mlaji. Pamoja na hilo Waziri Nagu alisema, uwepo wa kiwanda hicho ni sehemu ya vijana kujipatia ajira kwani wanatoa nafasi 50 za ajira.

Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu
Kitengo cha Mawasiliano
Tarehe 11 Novemba, 2014.
Mhe. Mary Nagu akipata maelezo akiangalia bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha kutengeneza Unga cha Basic Element Ltd Dar es Salaam.
Mhe. Mary Nagu akipata maelezo alipotembelea Kiwanda cha kutengeneza Unga cha Basic Element Ltd Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages