HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 11, 2014

Pepsi yaanzisha baahati nasibu kwa wateja wake

NA KENNETH NGELESI, MBEYA


KAMPUNI  inayo jihusisha  uzalishaji wa Vinywaji baridi nchini (Pepsi) SBC Limited Mkoa wa Mbeya imetangaza shindano  la jishindie mamilioni kila siku na Peps  kwa wakazi wa mkoa huo kwa lengo la kuwawezesha wananchi kujikomboa na hali ya kiuchumi.



Akizungumzia shindano hilo jana,Meneja mkuu wa SBC,Sanjay Munshi alisema kampuni hiyo imetangaza shindano hilo kwa lengo la kuwawezesha wananchi kujipatia zawadi mbalimbali zikiwemo soda na fedha taslimu kwenye soda.



Aidha Meneja huyo alibanisha soda ambazo zinazalihswa na kiwandoa hicho ambazo zitakuwa na zawadi kuwa  za Pepsi,Mirinda Orange,Mirinda Green Apple,Mirinda Fruity,Mountain Dew (300ml) na Seven Up zenye  ujazo wa 350mil.



Katika hatua nyingine Munishi alisema kuwa katika shindano hilo,wateja wataweza kujishindia kiasi cha sh 1,000,5,000,10,000 ambazo zitatolewa papo hapo mara baada ya mteja kupata zawadi hiyo.



Alisema kuwa  na kuwa kiasi cha sh.500,000,1,000,000 na milioni 2,500,000 zitatolewa kwenye ofizi za kampuni hiyo katika mikoa ya Dar es salaam,Morogoro,Lindi,Mbeya na Iringa katika muda wa kazi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 9 alasiri.



Munishi alisema kuwa  katika shindalo hilo ambalo litafiki tamati Jenuari 30 mwakami, kila siku kutakuwa na mshindi mmoja wa sh 1,000,000/ huku  akiweka wazi kuwa soda zenye bahati nasimu ni zile zenye vizibo vyenye rangi la dhahabu.



 Katika hataua nyingine Meneja huyo alisewma kuwa shindano hilo litahusisha mikoa 13 amabayo ni Dar essalaam,Mbeya,Morogoro,Pwani,Dodoma,Tanga,Lindi,Mtwara,Iringa Njombe,Rukwa,Ruvuma  na Katavi


Naye Meneja Mauzo wa kampuni Mkoa wa Mbeya Omari Jumbe, alisema katika shindano la bahati nasibu la kampuni hiyo ya SBC kwa mwaka jana jumla ya washindi 50 walijishindia zawadi mbalimbali na kuwa mwaka huu zawadi hizo zimeongezwa mara dufu kwa wateja.

No comments:

Post a Comment

Pages